Afisa mtendaji mkuu wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Dkt. Kamugisha
Kazaura ametoa mada kuhusu mkakati wa TTCL kusambaza mawasiliano ya kasi
katika majengo nchini wakati wa mkutano wa bodi ya Usajili wa
Makandarasi ( Contractors Registration Board (CRB) ambapo pia bodi hiyo
ilikuwa ikiadhimisha miaka kumi na tano tangu kuanzishwa kwake.
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na makandarasi takribani 800 kutoka
sehemu mbalimbali hapa nchini, Dkt. Kazaura aliwaeleza nia ya TTCL
kusambaza mawasiliano ya kazi katika majengo mbalimbali hapa nchini na
kuomba ushirikiano wa hali ya juu kutoka kwa makandarasi kujenga majengo
ambayo yatakuwa yamewezeshwa tayari kuunganishwa na huduma za
mawasiliano ya kasi " Broadband Ready Buildings".
Afisa Mtendaji mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura akiwasilisha
mada kwenye mkutano huo, kushoto ni Eng. Samuel D. Shila kutoka kampuni
ya Service Consult Ltd na kulia ni Bw. Mringi Kitaly kutoka Msafiri
Infrastructure and Mining Solution.
baadhi ya washiriki wakifuatilia mada hiyo kwa umakini.
Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura akifafanua
jambo kuhusu mkongo wa taifa wa mawasiliano kwa waandishi wa habari na
wateja waliotembelea katika banda la TTCL.
Dkt Kazaura (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa bi. Josephine
Mwakapugi kuhusu huduma zitolewazo na TTCL.
TTCL endeleeni kuupiga usingizi mnono. Anzisheni huduma za simu za mkononi na nyie pamoja na kutoa huduma bora wateje watakuja wenyewe.
ReplyDelete