Balozi Ramadhan Mwinyi Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, akizungumza wakati wa Mkutano wa Kudumu wa 12 wa Masuala ya Wazawa, katika mchango wake kuhusu mada ya utafiti uliofanywa kuhusu Ujasiri, Maarifa ya Jadi na Kujenga uwezo Jamii ya Wafugaji katika Afrika, Mwakilishi huyo ameeleza kwamba Jamhuri ya Muungano inajukumu la kuwaletea maendeleo wananchi wake wote na kwamba katika hakuna jamii itakayoachwa nyuma. Akasisitiza haja na umuhimu wa Jumuiya ya Kimataifa na wadau wengine kushirikiana na Serikali kufanikisha azma hiyo lakini pia kuunga mkono hatua na maamuzi inayoyachukua kwa manufaa ya wananchi wake na taifa kwa ujumla. Nyuma ya Balozi ni Bi. Ellen Maduhu Afisa wa Ubalozi .
Home
Unlabelled
HAKUNA JAMII ITAKAYOACHWA NYUMA KIMAENDELEO-TANZANIA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...