Na Abdulaziz Video
 Imebainishwa kuwa Muamko mdogo wa elimu miongoni mwa jamii Wilayani Ruangwa kunachangiwa na jamii wakiwemo Wazazi kutopenda kuchangia elimu ya watoto wao ikiwemo Ufuatiliaji wa nidhamu na maendeleo ya watoto wao.
  Akifungua kikao cha wadau wa Elimu wilayani humo,Mkuu wa wilaya ya Ruangwa,Bi Agness Hokororo alibainisha kuwa wilaya hiyo imejipanga kuhamasisha jamii kushiriki katika kuboresha elimu huku serikali ikijipanga kutoa motisha kwa walimu, mafunzo kazini pamoja na kutoa motisha kwa walimu wapya.
 Wilaya ya Ruangwa ina jumla ya shule 81 za msingi na 15 za sekondari ambapo kuna walimu 488 kati ya 673 wanaohitajika huku Shule za sekondari zina walimu 121 kati ya 256 na kati ya hao ni walimu 20 tu wa masomo ya sayansi na hisabati
 Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Agness Hokororo akifungua kikao cha wadau wa Elimu wilayani Humo kinachoendelea katika ukumbi wa Yongolo,Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya
Ruangwa,Clemence Mwakasendo na Kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya Bw Issa Njinjo
 Viongozi mbalimbali waliohudhuria katika kikao cha wadau wa ELIMU
 Wadau wa Elimu wilayani Ruangwa wakiwemo Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa
 Wadau wa elimu wakifuatilia kikao kwa makini
Kikao kikiendelea

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...