Meneja wa Programu ya Fanikiwa Kibiashara (BDG) Bw. Sosthenes Sambua (katikati) akiongea na Mhandisi Peter Chisawillo (kulia) na mkuu wa wilaya ya Nkasi, Bw. Iddi Kimanta (kushoto) wakati wa mafunzo ya kuwezesha kongano mbalimbali hapa nchini kujenga ubunifu na ushindani mjini Morogoro jana. Mafunzo hayo yanaendeshwa na Scandnavian Institute for Competitiveness and Development (SICD), Pan African Competitiveness Forum (PACF) na BDG, programu iliyo chini ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF).
Na Mwandishi wetu, Morogoro
Mfumo wa kongano bunifu umetajwa kama mkombozi utakaoleta maendeleo endelevu Tanzania kama utazingatiwa na wadau mbalimbali hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Programu ya Fanikiwa Kibiashara (BDG) ambayo inafanya kazi chini ya Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Bw. Sosthenes Sambua wakati wa mafunzo ya kuwezesha kongano mbalimbali hapa nchini kujenga ubunifu na ushindani mjini Morogoro jana.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...