Rais wa Marekani,Mh. Barack Obama.
Kuanzia tarehe 26 Juni hadi 3 Julai, Rais Obama na Mkewe wanatarajia kutembelea nchi za Senegal, Afrika ya Kusini na Tanzania.
Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.
Katika ziara yake hiyo, Rais atawekea mkazo umuhimu ambao Marekani inauweka katika ushirikiano wetu wa kina na unaoendelea kuimarika na nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia mipango mbalimbali ikiwemo ile ya kuimarisha ukuaji wa uchumi, uwekezaji na biashara, uimarishaji wa taasisi za kidemokrasia na uwekezaji katika kizazi kipya cha viongozi wa Kiafrika.
Rais atakutana na viongozi mbalimbali wa kiserikali, sekta binafsi na jumuiya huru ya kiraia ikiwemo vijana ili kujadili ubia wetu wa kimkakati katika ushirikano wetu rasmi na masuala mengine ya kimataifa.
Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla.
TAARIFA TOKA WHITE HOUSE, MAREKANI
Ziara hii itadhihirisha dhamira ya dhati ya Rais ya kupanua na kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na watu wa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara katika kuimarisha amani na ustawi katika kanda hii na duniani kote kwa ujumla.
TAARIFA TOKA WHITE HOUSE, MAREKANI
Mdau anony hapo juu mtaje tu ni William Malecela kuwa kaleta habariza uongo kuwa Kingunge Ngombare Mwiru hatunaye. Huyu jamaa ana matatizo ya inferiority complex. Hata ndugu zake nasikia haelewani nao. Maisha yamemshinda Marekani sasa kaja Tanzania kutuharibia mambo. Wadau Mwgopeni huyu mtu kama ukoma!!!
ReplyDeleteHehehe, Obama anakuja naona barabara zitapigwa deki
ReplyDeleteSijui mtaa gani utabadilishwa jina na kupewa jina lake? au sijui atapewa kiwanja kigamboni? au daraja la Kawe ,mlalakua litapewa jina lake?
ReplyDeleteWoiyeeeeee! Kichwa kinakuja kukazia Utandawazi/wizi. Na uwana Sesere wetu tumekwisha
ReplyDeleteIt is not kuja kuwasalimia tu. Huyo huenda mahali ambapo pana possilbe au kuna American interests. You have uranium. George Bush alitua bongo, hakuna cha ajabu.
ReplyDeleteTehe, tehe, tehe, Watanzania tumekwisha. Hawa mabepari sio size yetu na Hayati Mwalimu Nyerere alisema "MKINIONYESHA HUYO MJOMBA NITACHEKAAAAAA"
ReplyDeleteTumuombe Mungu hawa hawako kwa maslahi ya watanzania. Dunia ni kubwa.tehe, tehe, tehe, teheee!!
jamani! tusiwe na chuki na roho mbaya, mgeni anakuja kwako unawaza anakuja kukuibia, tuamke tujijenge sio kujisononesha, mbona mnaenda kwake kila mara! tumejazana wa tz ibao USA!
ReplyDeleteNafikiri tusiwe wakosowaji wa kila jambo na tusiwe tunaona kila jambo kwa negative attitude.. Ujio wake unafaida sana na of course hamna uwekezaji usiokuwa na bilateral benefit.. Kuna maendeleo makubwa tu ya mahusiano na nchi kubwa kama hii na wapo wengi wanaoutaka uhusiano huu.. Tuwaamini viongozi wetu tuliowachagua na pale wanapokosea tuwawajibishe
ReplyDeleteAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAKWISHNEI
ReplyDeletehuyu anakuja kutembea tu kwa vile ana asili ya Ki Africa sera ya Marekani zamani kusaidia Africa ni mambo ya ukimwi hakuna chengine.
ReplyDeleteMi nataka aje hasa atembelee na Zanzibar kule tena hiyo tarehe moja anokuja kuna bongo la mkutano daaahh
ANAKARIBISHWA KWA MIKONO YOTE ,KARIBU OBAMA NA NAMUOMBA AKAHUTUBIE BUNGE LA KITANZANI LA WALA RUSHWA WAJIFUNZE DEMOKRASIA MAANA YAKE NINI KARIBU SANA, KENYA MTAJIJU!
ReplyDeleteMimi naona akifika tu ,ule mtaa wa mbezi beach kuanzia Kawe keepleft baada ya Mwai kibaki iwe Jina Lake BARAKA OBAMA AVENUE, mpaka roundabout nyingine kwa Joseph Kusaga. Kwani huo ndio mtaa iliofanana na mindhali ya Marekani,
ReplyDeleteNa ule mtaa kutoka kona ya Africana kwenda white sand uwe WASHINGTON BOULEVARD. Hayo ni maoni yangu kwani naona tunakwenda tu kila siku marekani kama ndio MACCA yetu kwani kila mtu anaongelea huko tu ndio kama ibada yetu ya hivi sasa kwa hiyo naona tujipe moja kwa moja !
Tunakukaribisha sana nyumbani raisi Obama. Wewe ni shujaa, nasi watanzania tunapenda mashujaa, haijalishi policy zako zinapendwa huko Marekani au la, wote walio pita kabla yako walipendwa kwa mengine na kuchukiwa kwa mengine, Hata huku TZ viongozi wetu tuna wa treat hivyo hivyo, so karibu suijali, ulibadilisha historia ya watu wenye damu ya kiafrica marekani, sahizi dunia inatutazama kwa mtazamo mpya hahaaa.
ReplyDeleteIla kweli wazungu wanatisha, kwa unafiki tu hawajambo, huku ughaibuni nawatazama siwamalizi, wanakupenda wakijua kuna jambo watapata toka kwako, wezi wa idea ile mbaya, kwa kujitajirisha kupitia migongo ya wenzao (wanjonge) hawajaanza leo. Ila viongozi wetu wawe makini hakuna ku sign mikataba isiyoelewaka, wasikubali kushurutishwa, kama vipi tuache madini yetu yalale huko aridhini ikifika wakati vizazi vijavyo vikawa na uwezo wa kuyachimba na kunufaisha taifa, basi itakuwa vyema. Ni heri yabaki aridhini kuliko tuibiwe, ya toke kwetu, yachibwe na wana nchi wetu bila vifaa vya kujikinga waishie kupata saratani huko baadae, kufaidi wafaidi wengine, hizo nyakati zilisha pitwa na wakati sahizi tuko macho kweli kweli, kama unabisha uliza mtwara.
Kweli kabisa mgeni anakuja mkaribisheni kwanza kabla hamjamuhukumu..Karibu Obama kwetu Tanzania ukutane na ufisadi,wizi,uchochezi,uchonganishi na maugomvi yasiyo ya maana ya kidini
ReplyDeleteMTU MWEUSI HATAJIFUNZA HATA SIKU MOJA. HATA AKISAFIRI BADO USINGIZI WAKE NI MZITO SANA. SAMAHANI MICHUZI MIMI NASEMA WANA KHERI WALIOUKOSA UGENI HUU.
ReplyDeletemama weeeeeeeeeeeeeee madini yetu jamani ndio yanafuatwa sisi tutabaki maskini mpaka lini????????????????.Michuzi ugeni huu una walakini
ReplyDelete