Na Abdulaziz Video

IMEELEZWA kwamba zaidi ya watoto 15444 wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi mkoani Lindi wametambuliwa na wameanza kupatiwa huduma muhimu za kijamii kwa lengo la kuboresha maisha yao kupitia mradi wa pamoja tuwalee.

Hayo yamebainishwa na mratibu wa uwezeshaji uchumi kwa familia zinazoishi katika mazingira hatarishi mkoani Lindi kupitia shirika la PACT Tanzania,Rehema Madusa kwenye hafla fupi ya kukabidhi baskeli kumi na pikipiki moja kwa ajili ya wawezeshaji wa watoto hao wanaoishi kwenye mazingira hatarishi katika kata kumi za wilaya ya kilwa.

‘watoto hao waliotambuliwa wanalelewa na walezi 2617 wakiwemo wanaume 480 na wanawake 2137 kutoka vikundi 192 vilivyo undwa kutokana na familia duni za watoto hao kutoka kila wilaya Kwa mujiu wa mratibu huyo mpango huo wa pamoja tuwalee wa miaka mitano ulianza kutekelezwa mwaka 2010 ukiwa na malengo saba kwenye maeneo ya elimu,afya na lishe, ulinzi wa watoto, msaada wa kisaikolojia,msaada wa kisheria, hifadhi ya jamii, na huduma ya kuboresha kipato.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...