Ndugu zangu waTanzania
wenzangu,
Sisi watanzania wapigania
maendeleo - CHADEMA UK tumelazimika kuwasilisha majonzi yetu kwenu kwa njia
hii, ikiwa ni katika kuonyesha mshikamano wa kitaifa kwa kujifariji na pia
kuwafariji ninyi waTanzania wenzetu kutokana na tukio kubwa la kuhuzunisha sana
ambalo limetokea hivi majuzi nchini mwetu huko mkoani Arusha.
Pamoja na kwamba pamekuwa na
matukio kadhaa yaliyoikabili nchi yetu hili la Arusha tumeonelea tulisemee kwa
njia ya kipekee,kwa sababu licha ya kwamba ni tukio la kigaidi, lisilokuwa na
mantiki yeyote ile zaidi ya umwagaji damu wa raia wasio kuwa na hatia,bali pia
utekelezwaji wake unaweza kutuachia athari kubwa sana kisaikolojia na
kimahusiano kama tusipojaribu kulitathmini na kulitafakari kwa upekee wake.
Wakati ambapo sala na maombi yetu
kwa sasa yawaeendee wafiwa na wale ambao wamedhurika moja kwa moja kimwili ama
kisaikolojia kutokana na tukio hili, tunapenda pia kupongeza juhudi
zilizofanywa na kila mmoja wetu aliyeweza kuwafikia na kutoa msaada wa aina
moja ama nyingine kwa wahanga wa janga hili bila kujali tofauti ya vyama, itikadi,
kabila, dini ama falsafa. Hiyo ndiyo Tanzania tunayoijua sisi. Pamoja na
tofauti zetu nyingi ki hali,afya ama kipato, lakini kamwe hatubaguani katika
misingi ya rangi, kabila ama dini. Na hili ndio haswa linalotusukuma sisi kuwasilisha
huu waraka wa rambirambi kwenu ninyi wenzetu leo hii.
Tuna imani kwamba vyombo
vyetu vya usalama vitafanya utafiti wa kina kuchimbua na kutujuza chanzo cha
ufedhuli huu, ni lazima sisi wenyewe pia tufarijiane kwa maombi, michango na
tafakuri mbalimbali zenye kutiana moyo katika kipindi hiki kigumu kwetu sote.
Tuna imani kwamba yeyote aliyehusika katika mkakati huu atapatikana na kupewa
adhabu inayostahili.
Kwetu sote watanzania, huu ni
wakati muafaka kuonyesha mshikamano wetu kuwatumia ujumbe hao wachache wenye
nia mbaya kwamba waTanzania tumeundwa kutoka jumuiya ya makabila zaidi ya mia
moja, wenye asili, rangi, dini na madhehebu mbalimbali na wasioamini. Na kati
yetu wote sisi ni marafiki na ndugu, wengine ni ndugu wa damu kabisa, kupitia
ndoa, wazazi n.k. Hivyo sisi hatuwezi kubaguana wala kuwa na chuki miongoni
mwetu kwani hiyo si asili yetu. Na yeyote yule atakayejaribu kupandikiza mbegu
hii chafu miongoni mwetu tumkatae na kumchukilia hatua stahiki kumtokomeza yeye
na kundi lake.
Ujumbe wetu kwa watanzania ni
huu:
HII NI VITA DHIDI YA UMOJA
WETU WA KITAIFA NA SIYO KUNDI AU IMANI FULANI.
Asanteni sana,
Mungu
awabariki nyote.
Mungu alibariki taifa letu Tanzania.
Kwa niaba ya CHADEMA UK
G Mboya
Secretary
Hiiimetulia wakubwa! nawakubali!
ReplyDeleteKwa hakika ni ujumbe murua ulio na sura ya kitaifa.Huo ndio utanzania,na kwa hakika ndivyo hasa tunavyopaswa kuishi.MUNGU ibariki nchi yetu.
ReplyDeleteMpaka sasa hakuna ukakika kamili kama ni vipi:
ReplyDelete1.Pana mivutano ya Waumini wa Dini ndani kwa ndani Makanisani Arusha,
-Pana Mogogoro wa muda mrefu wa KKKT tulishuhudia silaha za moto zikitumiwa ktk mgogoro miaka ya 1997-1999,
-Pana Kibwetere mmoja wa Kanisa la Kilokole Arusha alichangisha waumini Mil. 500 halafu akafanyia mipango isiyoeleweka, wauimini wakaja juu.
2.Siasa za Jazba zimetawala sana ktk Arusha ya sasa.
Arusha sasa ni mji wa maandamano kila kukicha, biashara hazifanyiki ipasavyo tofauti na ilivyokuwa zamani Arusha ilikuwa ni mji wa fedha na sasa ni mji wa Siasa za chuki na visasi.
Hivyo kwa msingi huo hatuwezi kujua kwa haraka inawesekana ni ktk hili.
3.Waarabu wageni Raia wa Saudi Arabia waliokamatwa na kushikiliwa ni kuwa sio watuhumiwa isipokuwa wanafanyiwa uangalizi kwa kile walicho onekana wakisafiri kuelekea Nairobi siku moja baada ya tukio...tusije tukajenga mtazamo wa moja kwa moja dhidi ya Misimamo ya Kigaidi kutoka kwa Waarabu kwa kuwa ''wavumao ni wachache, lakini na wengine wengi wamo pia''
Nia waTZ tunayo ya kulindaa umoja wetu. Lakini wachache wenye nguvu zao wanatuharibia.Kuna mdau mmoja kwenye blog hii aliandika" ukiona kero imeshindikana kutanzuliwa ujue kuna kigogo nyuma."
ReplyDeleteAliendelea kutoa mfano wa ajali za barabarani. Haziishi kila kukicha. Madereva hawako tayari kufuata sheria za barabarab. Kumbe wenye magari ni maafande, mawaziri , wabunge n.k
Na huu ugaidi hauko mbali kukamata. Itategemea atakayekubali kumfunga paka kengele.
Hakika huu ujumbe umeandikwa na Mtanzania wa kweli. Naomba wachangiaji tuache kupotisha maana ya ujumbe huu. Tuwaze Kama Watanzania natuache kuweka maslahi binafsi mbele. Mungu atusaidie Uzalendo wa enzi za Mwalimu urudi tena!
ReplyDeleteNinyi mnaotoa MAKALA hii mrudi TZ na siyo mbakie huko Uingereza wakati chama chenu kinafanya vibaya nchini na hasa hukohuko Arusha ambako kumekuwa ZAIDI YA DODOMA KWENYE MAKAO MAKUU YA SERIKALI NA BUNGE ni kuwa ARUSHA YA SASA IMEGUBIKWA NA SIASA KAMA MDAU WA 4 ANAVYOSEMA.!!!
ReplyDeleteMlitakiwa Makada wa Chama mshuke kutoka huko UK mtinge Arusha ili kukinusuru chama chenu kinacho boronga kila kukicha na sio kutoa makala pekee!
HAPO NDIPO TUTAMKUMBUKA MWALIMU, NA TUSIMUONE. UONGOZI SIO MCHEZO.MWL ALISIMAMA KWA WAKOLONI NA KWA MAKABURU NA TUKASHINDA. JE, VIONGOZI HAWA WA SASA WANASHINDWA VIPI KUTHIBITI HALI YA USALAMA NDANI YA NCHI? KAMA MDAU ALIVYOSEMA HAPO JUU, JUU YA AJALI BARABARANI! NA SASA WATU KUUWAWA OVYOOVYO TU! JE,KAMA WATU WANAUWAWA MUTAONGOZA NANI KESHO?
ReplyDelete