Wachezaji wa timu za Taswa FC (wenye jezi za bluu) pamoja na wapinzani wao wa Bongo Movie,wakisikiliza kwa makini maelekezo toka kwa refarii wa mchezo huo ambaye alikuwa ni Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya,Ally Kiba (kushoto) muda mfupi kabla ya kuanza kwa mtanange wao ulipigwa kwenye Viwanja vya Sigara (TCC),Chang'ombe jijini Dar es Salaam jana jioni.Mtanange ulikuwa ni mkali sana kwa pande zote mbili na hadi mwisho wa mchezo timu ya Bongo Movie iliibuka kidedea kwa bao 2 - 0.hii ikiwa ni kwa upande wa mpira wa miguu lakini katika mpira wa pete,timu ya Taswa Queens iliibanjua timu ya Bongo Movie kwa Mabao 38 - 10.
Straika wa timu ya Taswa FC,Juma Pinto akichuana vikali na Beki wa timu ya Bongo Movie (ambaye hajawahi kuonekana kwenye movie) wakati wa mtanange wao uliopigwa jana jioni kwenye Viwanja vya Sigara (TCC),Chang'ombe jijini Dar es Salaam.
Watazamaji upande wa Taswa FC.
Watazamaji upange wa Bongo Movie.
hapa ni bambi kwa bambi,huku Refa akiangalia kwa makini kuona kwamba hachezewi mtu faulo.
Taswa FC kwa chenga tu hawajambo.
Mtanange mkali kati ya Taswa Queens dhidi ya timu ya Bongo Movie ukiendea kwa kwa kasi.hadi mwisho wa mchezo huu Taswa Queens iliibuka kidedea kwa Mabao 38 - 10.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...