Na Mahmoud Ahmad Arusha
Wagonjwa saba ambao ni majeruhi wa mlipuko wa bomu kwenye kanisa la Joseph Mfanyakazi eneo la Olasiti jijini Arusha wamehamishiwa kwenye Hospitali za Muhimbili na LUgalo jijini Dar es Salaam.

Majeruhi hao wamesafirishwa mchana majira ya saa tisa kwa ndege ya shirika la Hifadhi za taifa (TANAPA) kwenda kuendelea na matibabu zaidi baada ya hali zao kuonekana bado zinahitaji vifaa vyenye uwezo wa hali ya juu.

Miongoni mwa walisafirishwa wapo watoto watatu wakike wawili na wakiume mmoja huu wakina mama walisafirishwa wakiwa wawili na kinababa wawili ambao hali zao bado mbaya licha ya matibabu walikuwa wakiyapata tokea juzi.

Wasamaria wema kutoka makampuni mbali mbali wameendelea kutoa misaada mbali mbali ya hali na mali ikiwemo madawa na vifaa tiba na mablanketi na mashuka,na Magodoro iliviisaidie hospitali za Mt.Meru na St,Elizabeth.

wakati huo huo wabunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania wamewatembelea wahanga wa bomu na kutembelea kanisa ambalo yalitokea maafa na kujionea hali halisi wakiongozwa na spika wa bunge hilo Anna Makinda

Miongoni mwa wabunge hao ni Mh.Habibu Mnyaa ambaye alisema kuwa hali kama hiyo imewatia simanzi na kuiomba serekali kuchukuwa tahadhari kubwa kwa matukio kama haya akiongea mbunge wa viti maalumu ccm vijana Catherine Maggige alsema kuwa majeruhi hawa wanatia huruma na kuwa kitendo hicho kilichotokea hakliwezi kuvumilika na kuiomba serekeli kuchukuwa hatua za haraka kukabiliana na wimbi la tukio kama hilo.

Kwa upande wake spika makinda hakuweza kutoa neno lolote bali aliingia kweny Gari teyari kwa safari ya kurudi Dodoma huku akiwa na huzuni kubwa.
mtoto akiwa amebebwa na baba yake huku akipokelewa na nesi wa hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya kupelekwa kiwanja cha ndege cha Arusha kwa ajili ya kusafirishwa kupelekwa katika hospitali ya Taifa ya Mmuhimbili jijini Dar es Salaam kwa matibabu
wagonjwa walioathirika na bomu la kurushwa jumapili iliyopita wakiwa wanapandishwa kwenye gari ya wagonjwa tayari kwa kupelekwa katika kiwanja kidogo cha ndege cha mkoa arusha kwa ajili ya kuamishiwa katika hospitali ya muhimbili jijini dar es salaam. Mahmoud Ahmad Arusha.Picha na Woinde Shizza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 09, 2013

    Mara Kwa mara tunasoma kwamba viongozi wetu wa Tz na wenye nazo wakiumwa husafirishwa kwenda nje ya nchi eg.India na South Africa kwa ajili ya matibabu. Now I Wonder!Dar tuna hospital nzuri, za kuaminika sana, ambazo sio private hospitals? Why do those People fly abroad for treatments?

    ReplyDelete
  2. Aah innocent people.may God give then strength and let them get well soon.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...