Kamera ya Globu ya Jamii,imemnasa mtu huyu ambaye ni omba omba akiwa amekaa katikati ya barabara ya Bagamoyo karibu kabisa na eneo la Victoria jijini Dar es Salaam, akiomba kwa watu wanaopita na magari katika barabara hiyo. Jambo hili si salama sana kwa mtu huyu kwani lolote linaweza tokea japo hatuombei itokee,hivyo ombi kwa wazee wa feva (wanausalama barabarani) kusaidia kumuondoa huyu mtu mahala hapa haraka iwezekanavyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 07, 2013

    Huyu jamaa sio ombaomba ni kichaa. Alikuwa anasimama anatembea mbele kisha anageuza na kurudi, anaweza kufika tegeta kwa huo mzunguko. Sasa hv anakaa hapo barabarani. Alikuwa na manywele marefu sana na machafu naona wasamaria waliamua kumnyoa. Ni wakusaidia na kupelekwa hospitali.

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 07, 2013

    Huyu jamaaa ndo kijiwe chake hapo victoria miaka nenda rudi hata wakimtoa kesho atarudi

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 07, 2013

    Wakati umefika kwa serikali kuanza kutoa "Benefit" kwa walemavu.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 08, 2013

    Mdau wa BENEFIT umenichekesha na kunikumbusha mbali sana....kama huku uingereza kwenu mnakatiwa benefit itakuwa bongo?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...