Dear Ankal
Kwa kweli wajumbe wa tume ya katiba wameyatendea haki maoni ya watanzania juu ya katiba mpya. Ingawa sijapata muda wa kusoma kifungu hata kifungu kwa utulivu, lakini kwa muonekano wa awali rasimu ni nzuri na itahitaji marekebisho machache ya kimsingi. Rasimu ya katiba imependekeza kuwepo kwa serikali tatu, yaani ya Muungano, ya Tanzania zanzibar(ambayo ipo kwa sasa) na ya Tanzania Bara( ambayo katika katiba ya zamani imo ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania). Kwa utaratibu wa tume rasimu ya katiba itajadiliwa katika mabaraza mbalimbali yalioundwa katika ngazi tofauti na baadae kwenye bunge la katiba na mwishowe itapigiwa kura ya maoni na itakuwa tayari mwaka 2014. Serikali , inataka katiba hii ianze kutumika katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Angalizo langu:
Iwapo katiba hii itapita katika mchakato mzima na ikakubalika kwa wananchi kwamba tuwe na serikali tatu. Serikali ya Muungano itakuwa na katiba, Serikali ya Tanzania Zanzibar wanayo katiba yao, Serikaliya Tanzania bara itakuwa haina katiba yake, hivyo basi tutabidi tuanze mchakato mpya wa kupata katiba ya serikali ya Tanzania bara mwaka 2014. Hili linaweza kuchukua muda mrefu na pengine kuchelewesha au kuhairisha uchaguzi wa mwaka 2015.
Sijui serikali na wanasiasa wanaliangaliaje hili.
Wadau wa Globu ya Jamii je mna mawazo gani kuhusu angalizo hili?
Mdau wa KATIBA
Kwa kweli wajumbe wa tume ya katiba wameyatendea haki maoni ya watanzania juu ya katiba mpya. Ingawa sijapata muda wa kusoma kifungu hata kifungu kwa utulivu, lakini kwa muonekano wa awali rasimu ni nzuri na itahitaji marekebisho machache ya kimsingi. Rasimu ya katiba imependekeza kuwepo kwa serikali tatu, yaani ya Muungano, ya Tanzania zanzibar(ambayo ipo kwa sasa) na ya Tanzania Bara( ambayo katika katiba ya zamani imo ndani ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania). Kwa utaratibu wa tume rasimu ya katiba itajadiliwa katika mabaraza mbalimbali yalioundwa katika ngazi tofauti na baadae kwenye bunge la katiba na mwishowe itapigiwa kura ya maoni na itakuwa tayari mwaka 2014. Serikali , inataka katiba hii ianze kutumika katika uchaguzi wa mwaka 2015.
Angalizo langu:
Iwapo katiba hii itapita katika mchakato mzima na ikakubalika kwa wananchi kwamba tuwe na serikali tatu. Serikali ya Muungano itakuwa na katiba, Serikali ya Tanzania Zanzibar wanayo katiba yao, Serikaliya Tanzania bara itakuwa haina katiba yake, hivyo basi tutabidi tuanze mchakato mpya wa kupata katiba ya serikali ya Tanzania bara mwaka 2014. Hili linaweza kuchukua muda mrefu na pengine kuchelewesha au kuhairisha uchaguzi wa mwaka 2015.
Sijui serikali na wanasiasa wanaliangaliaje hili.
Wadau wa Globu ya Jamii je mna mawazo gani kuhusu angalizo hili?
Mdau wa KATIBA
Serikali tatu ni mzigo kwa Wananchi wa Tanzania Sio Jambo la kushabikia hata kidogo, Katiba bora ni ile itakayoleta unafuu kwa Wananchi wa Taifa husika, kwa kipindi cha Muda mrefu huduma za Afya, Elimu na Miundombinu mingi imekuwa ikitengewa fedha kidogo kutokana na ufinyu wa Bajeti, sasa mfumu wa Serikali Tatu, maana yake hata ile bajeti ndogo itatumika kwa Ajili ya kuendesha Serikali badala ya kuleta Maendeleo. Ni vyema tuwe na Serikali Moja ambayo itakidhi mahitaji ya wananchi, ambayo itaboresha huduma muhimu pamoja na kuongeza fursa za kiuchumi kwa Wananchi.
ReplyDeleteRasimu ya Katiba, itawanufaisha wanasiasa wanaotaka uongozi, na Si wa Wananchi weye kiu ya Maendeleo.
TUSEME HAPANA KWA SERIKALI TATU, TUNATAKA SERIKALI MOJA, NA HIYO NDIO MAANTIKI YA KUUNGANA KWA NCHI MBILI
mie nakubaliana na mdau wa hapo juu kabisa,kwamba itakuwaje nchi mbili ziungane halafu kupatikane marais wa tatu? kwanini kusiwe na serikali moja ? tu tumeungana kivipi sasa mbona sielewi? kila mwaka nchi ndogo itakuwa inafanya kutafuta viongozi wa ngazi mbali mbali kutokana na kuwepo kwa madara sana,mie naona hapo serikali moja tu basi ,kama haiwezekani wapeni zenji nchi yao bana
ReplyDeletena sisi wazanzibari tunasema hatutaki serikali mmoja tunataka mbili kwa sababu tulivyo ungana tulikuwa serikali huru na kwanini tupoteze uhuru wetu kwa ajili ya kuungana
ReplyDeletewatanganyika tafuteni serikali yenu
msidhani sisi wajinga tumekaa kimya lakin tuna jua kutafakari kwa kina kirefu sana
tumechoka kutawaliwa tuna taka taifa letu huru lenye heshma na hadhi ya nchi huru hatutaki muungano tena
kila mtu anamtazamo wake. Serikali tatu ni kuwadanganya wazanzibari kwa kifupi. Hio serikali ya muungano na ya tanganyika imechanganywa humo humo ktk serikali ya sasa ya muungano.
ReplyDeleteNa ikiwa hizo wizara muhimu ambazo wazanzibari hawataki ziwe kwenye muungano bado zitabakia kwenye serikali mpya muungano , basi hakuna haja ya kuwa na serikali tatu.
Tunasema tena hatutaki muungano kila mtu awe na serikali yake , tuwe na ushirikiano tu kama vile tunavyoshirikiana na uganda , kenya nk. Hawa kina warioba wasidanganye wazanzibari bure wanajidanganya wenyewe , wenye macho hawaambiwe watazame. Wenye akili ni wengi lakini maarifa ndio tatizo , tunakuomba warioba na tume yako chukueni wenyewe hio katiba. Na kama waadilifu basi tuipigie kura. waznz hawataki muungano basi mmetushika tuuuu , heee
Kusema kweli kwa rasimu hii bado ni danganya toto ila WAZANZIBAR waleo sio wa jana hakuna mzanzibar mjinga akubalie kuburuzwa tena tushachoka kila siku kupangiwa tunataka tujiendeshe wenyewe hio rasimu ni usanii tu wa kutaka kuendelea na katiba hii hii kwa sababu wanajuwa hakuna atakaekubali huo ujinga wao na mara hii ni mwisho ikishindikana kukubaliana na kile tukitakacho mamlaka kamili zanzibar mamuzi magumu tutakayoyachukua potelea mbali :LIKITOTA NALITOTE : KWANI LAZIMA TUUNGANE TUSHASEMA HATUTAKII HEBU TUACHIENI NA KIJINCHI CHETU .
ReplyDelete