Ndugu Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Wakazi wa kijiji cha Malangali,Kata ya Luduga,Wilaya ya Wanging'ombe mapema jana jioni.Kinana alizungumza mambo mbalimbali ikiwemo na suala la mgogoro ardhi uliohusu wananchi waishio eneo la hifadhi ya Malangali kuhamishwa,Kinana aliishauri serikali kulifanyia kazi jambo hilo kwa umakini mkubwa, kuondoa mgongano na usumbufu kwa wananchi,Aidha katika mkutano huo hadhara Kinana aliahidi kiasi cha fedha kwa vijana kuwawezesha kuunda umoja wao wa kufanya shughuli mbalimbali za kimaendeleo. 
Maelfu ya wananchi wakimlaki Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (chini ya bendera) alipowasili jana, kwenye Ofisi ya CCM Wilaya ya Wanging'ombe, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama mkoani Njombe.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akishiriki kuchanganya udongo kwenye ujenzi wa zahanati ya Samaria, Kata ya Makoga Wilaya ya Wanging'ombe alipopita eneo hilo, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM, kukagua na kuimarisha uhai wa Chama mkoani Njombe.
PICHA ZAIDI BOFYA MICHUZIJR.BLOGSPOT.COM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 01, 2013

    Chdm mkisaidiana na Mhe. P. Msigwa mkachane mbao msituni!

    Iringa yote na Wanging'ombe hizoooo mikononi mwa CCM

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...