![]() |
Profesa Said A Mohammed |
SEHEMU YA KWANZA
Profesa Said A Mohammed umeandika vitabu vingi.
Ama kweli wewe ni hazina ya fasihi ya Kiswahili ambaye hujapata heshima
inayokustahili. Najua hupendi kusifiwa – lakini lazima tukuthamini ungali hai
maana wewe fahari yetu Waswahili. Hata ukiweka neno “Tanzanian Novelists”,
“Zanzibar Writers”, au “Tanzanian Writers” katika Wikipedia hutajwi. Unadhani
kwanini wengi hasa Tanzania bara na
visiwani hawakufahamu ipasavyo?
Mwandishi : Said A Mohammed
Kama nilivyokueleza katika mkumbo wa
masuali uliyoniuliza mwanzo hapo kitambo, Watanzania na zaidi Wazanzibari
hawana utamaduni wa kusoma vitabu vya fasihi. Kwa hivyo hawajapata ari wala
mwamko wa kujali na kuthamini fasihi yenyewe na waandishi wake. Kweli kuna
wachache ambao wanatangazwa katika vyombo vya mawasiliano, lakini mimi simo
katika orodha ya waandishi hao. Hili ni suala la vyombo vya habari ambavyo mara
nyingi huwatukuza wale ambao wanataka wao watukuzwe.
Vilevile kuna wasanii
wanaopenda kujipeleka mbele ili wasikike na hata kuwa na fikra kwamba waandishi
wengine wadidimie. Kwa bahati mbaya au labda kwa bahati nzuri, mimi si mtu wa
kimbele mbele. Naamini sana maneno ya wahenga kwamba Kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza.
Katika dunia ya sasa kujipeleka mbele ili usikike bila umakinifu, ndilo
jambo linaloharibu mambo mengi ikiwemo sanaa ya lugha.
Vipawa vinadharauliwa na
sanaa tunazokutana nazo ni sanaa zinazokuzwa tu bila ya kupitiwa kwa kina na
kujadiliwa. Chambilecho, gwiji wetu wa fasihi, Profesa Ebrahim Hussein, hakuna
fasihi tena kwa maana ya fasihi. Hakuna wasomaji wazingatifu. Hakuna uhakiki
kwa maana ya uhakiki. Kuna fikra ya kwamba chochote kile ni sawa. Shairi,
riwaya, hadithi fupi au tamthilia ikiwa ina sura ya tanzu inayohusika, basi ni
fasihi tu kwa maoni ya wengi.
Fasihi
haipo. Wasomaji hawapo. Umakinifu wa fasihi haupo. Uhakiki umepotea. Hata wale
ambao tunawatarajia kufanya hivyo hawashughuliki na kusoma, kuandika, kuhakiki
na kuzitangaza kazi za fasihi ya Kiswahili. Sisi waandishi hatuwezi kujitetea.
Wanaojitetea na kuwaponda wenzao ndio katika hao wanaowekwa mstari wa mbele na
wanaojitapa kuwa wanajua hata kuandika kazi za waandishi wenzi wao. BOFYA HAPA KUSOMA MAHOJIANO YOTE
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...