Instabul,Uturuki: Baada ya maandamano ya wiki tatu katika mji mkuu wa Istanbul,nchini Uturuki, Mapema leo wandamanaji waliamrishwa kuondoka mara moja katika viwanja vya Taksim Square,Istanbul,amri hiyo ilitolewa na meya wa mji huo Bw. Huseyin Avni Mutlu.

Meya huyo aliwataka wandamaji waondoke katika viwanja hivyo ili usafi uweze kufanyika wa kusafisha eneo hilo,lakini wandamanaji waliendeleza libeneke la maandamano,Waziri mkuu wa nchi hiyo Bw.Tayyip Erdogan amekubali kuonana na viongozi wa maandamano hayo siku ya jumatano na kusikiliza matakwa yao,lakini kabla ya viongozi hao kuonana na waziri mkuu wa nchi hiyo.

Askari wa kutuliza ghasia (kina Ras makunja) wa nchi hiyo wameshavamia viwanja vya Taksim Square na kuwarushia wandamanaji milipuko ya machozi,maji ya kuwasha na mkong'oto kama ilivyo mila na desturi yao kina ras makunja(FFU).

kina ras makunja wa uturuki wakipereka na muziki wao hewani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2013

    MAMBO YA UTURUKI HAYATUHUSU.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2013

    Mambo Uturuki yanatuhusu dunia imekuwa kijiji,watanzania kuna vitu vingi vya kujifunza,kenya walipopata matatizo tulisema hayatuhusu...baadaye nasi yalituka

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...