Askari kanzu (kulia) akiwa ameshika bastola aliyokutwa nayo mtu mmoja aliyekuwa amepakiwa katika pikipiki aina ya Boxer yenye namba za usaji T 961 CJW katika mtaa wa Makunganya jirani kabisa na benki ya Posta jijini Dar es Salaam mchana huu. Kutokana na kuongezeka kwa matukio ya ujambazi wa kutumia pikipiki Polisi wameimarisha ulinzi na hasa katika maeneo ya mabenki. 
Asklari kanzu akiwa na bastola alikamatwa nayo mtu mmoja aliyekuwa amepakiwa katika pikipiki aina ya Boxer.
 Watu waliokamatwa wakijaribu kuwasiliana na ndugu zao.
 Neno kwenye Pikipiki waliyokuwa wakitumia hao. 
 Ofisa wa Polisi akijaribu bastola waliyokutwa nayo watu wawiliwaliokuwa katika Pikipiki Posta Mpya jirani na Benki ya Posta leo.
 Heee ina risasi!
 Mtu aliyekutwa  na bastola hiyo, ambaye alijitambulisha kama mfanyabiashara.
 Polisi wakifanya mawasiliano na wenzao wa doria kuomba msaada wa gari.
 Mtuhumiwa aliyekutwa na bastola akihojiwa na kuchukuliwa maelezo.
 Dereva wa Pikipiki naye akichukuliwa maelezo yake.
 Unaitwa nani, unaishi wapi, unafanya kazi gani, kabili gani, Ofisa wa Polisi akimuhoji mtuhumiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 30 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 25, 2013

    Nimependa hilo neno kwenye pikipiki

    ReplyDelete
  2. Walijuaje km anabastola km c mwajuana sasa mwaanza kugeukana kwenye saliyo

    ReplyDelete
  3. Sasa hawa mapolisi kanzu mkianza kuwaanika hapa si waarifu watawatambua bwana. Funika uso kidogo na photoshop.

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 26, 2013

    haha wamekamatwa na bastola lakini wamekaa kama marafiki na hao polisi hata wasiwasi hawana na polisi wanawapa ruhusa ya kuwasiliana na simu kama kawaida kweli bongo muozo

    huku ughaibuni ukikamatwa kwa kosa lolote au kushukiwa na jambo lolote kitu cha kwanza wanakusachi mifukoni wanachukua kila kitu chako na ukifikishwa kituo cha polisi hupewi nafasi ya mawasiliano ya simu mpaka baada ya siku 3 kwa maana hiyo muda huo wote watakapokuwa kwenye uchunguzi hutoweza kuwasiliana ili kuharibu uchunguzi wao

    sasa hapo bongo watuhumiwa wanaruhusiwa kuongea na simu ili wajipange na watu wao kujenga majibu kwenye maswali watakayoulizwa ili ionekane walikuwa hawana nia mbaya.

    bongo badobado sana labda mpaka 2050.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 26, 2013

    kidhibiti kinashikwashikwa tu ovyo namna hiyo kweli

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 26, 2013

    kidhibiti kinashikwashjikwa tu ovyo namna hiyo duh

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 26, 2013

    Hiyo nimewipenda tena muwakague vizuri humo kwenye mifuko wanamabomu pia, halafu muulizeni pia yule mwenzake alielipua Bomu kule Arusha yuko wapi? na aeleze vizuri.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 26, 2013

    Wee unakaa ughaibuni ipi ambyo mtu akikamatwa haruhusiwi kuwasiliana na wenzake.

    Wacheni kudanganya watu na ughaibuni yenu.Hayo wameanza leo!

    N polisi wakikamata haya wanaanza kuumbuana na watu wanaojuana nao,wasipokamata polisi wa bongo hawajui kazi.watu mnasikitisha sana hata hamwleweki mnataka mvua au mnataka jua.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 26, 2013

    Hizo zinauzwa kama njugu sasa kila mtu anayo, akifika police atatoa risiti aliyonunulia basi, sheria ina mruhusu kutembea nayo

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 26, 2013

    Mdau uko ughaibuni gani? Ambako mtuhumiwa hana haki hata ya kuwasiliana na wakili wake? Na hivi mnajudge vipi kosa kwa picha? Kwani kuwa na bastola ni kosa? Hebu vyombo vya habari kuweni na weledi, fanyeni uchunguzi, muwahoji polisi maswali ya msingi na muandike kitu cha kueleweka!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 26, 2013

    KAMA SIO MCHEZO WA KUIGIZA BASI HONGERENI SANA POLISI. LAKINI HAO WOTE WANATAKIWA WASHUSHWE VYEO KWASABABU KUANZIA LEO SIO ASKARI KANZU..WAMEKUA ASKARI WAAAZI. HATA MIMI NA WEZI WOTE WAMEAWATAMBUA. PILI WALIBEBA WAANDISHI WA HABARI KUCHUKUA TUKIO? WALIJUAJE HAKUTATOKEA MAPIGANO? LAKINI KAMA MWINGINE ALIVYOSEMA UTAMPAJE MUDA AWASILIANE NA SIMU???? HIYO SIMU INATAKIWA IWE SEHEMU YA UCHUNGUZI. UKITILIA MAANANI KUWA KUNA MATUKIO MENGI YA WIZI WA SILAHA KWA KUTUMIA PIKIPIKI?? HATA HAWA ASKARI WACHUKUIWE HATUA.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 26, 2013

    Bado hatujafika.Askari anashika bila gloves sasa hizo finger prints ?Cha ajabu zaidi badala ya kwenda kituoni kuwauliza kupata habari kamili wao kila kitu hapo mtaani .Jamani sihata wawe wanaangalia mves zenye juh kazi zao wajifunze

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 26, 2013

    Hawa jamaa wanaonekana si majambazi hiyo Bastola ni ya kujilinda wao wenyewe .. Jambazi ukiliona tu unalijua.. Watu wenyewe hata wasiwasi hawana bana. Labda am so naive to judge people according to their looks but the body language tells the all story, am convinced these people are legally gun holders.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 26, 2013

    hee sasa wakikana mahakamani kama sio yao wapepandikiziwa tu na polisi tizama fingerprint polisi si watakuwa wamekwisha mmhhhh bongo kunaendeshwa ki kariakoo kariakoo tu.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 26, 2013

    Anony wa nne toka juu umesema kweli. Kumpa mtu ruksa ya kuongea na simu mara baada ya kutuhumiwa sio jambo la maana. Ukitembea na siraha lazima uwe na kibari chake. Askari kanzu munaweza kusitukia munavamiwa! Harafu hapo hapo hawa watuhumiwa wangepigwa pingu chapu chapu. Kweli Bongo......

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 26, 2013

    wapi mnafahamiana nyie,sema upande wa salio ndo zengwe hapo!

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 26, 2013

    Kwani mtu haruhusiwi kuwa na bastola kama ameichukua kihalali? Tusitoe majibu kabla ya polisi kwani yawezekana wanamiliki kihalali. Tusibiri majibu ya polisi ndipo tutoe tuhuma, sio mnakurupuka tu.

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 26, 2013

    YANI HAWA WANAOPAKIZANA WATATU KWENYE PIKIPIKI MARA NYINGI NI WAARIFU HII NIMESHUHUDIA JUZI,NILIKUWA NIMEPITA MITAA YA MIKOCHENI NILIKUWA KWENYE USAFIRI BINAFSI,GAFLA NIKASIKIA KISHINDO KIKUBWA SAANA KUMBE WALE JAMAA KUNA KIJANA ALIKUWA NA BODABODA HUWA ANATOKA KWENYE BIASHARA FLAN WAMEMSOMA,JAMAA ALIVYOVYATUA YA KWANZA ANATAKA KUFYATUA YA PILI,ILE BASTOLA IKAANGUKA CHINI WA BAJAJI AKAIOKOTA IKABIDI WA PIKIPIKI WAKIMBIE

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 26, 2013

    Kwani mtu huruhusiwi kutembea na bastola yako unayomiki kihalali? mbona watu kibao sana wanazo mjini na wanajulikana, mbona hawakamatwi, au ndo mlijua kuwa hao jamaa wanataka kufanya uhalifu? sijaelewa!

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 26, 2013

    Siku hizi Tanzania huwezi hata kwenda bank maana ukitoka hata na million moja unapigwa risasi una tolewa uhai wako!!!! Watu wa Bank wana wasiliana na watu wabaya/majangili halafu unanyang'anywa pesa na kuuliwa na watu waendeshao piki piki. Haya wawataje na wenzao sasa.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 26, 2013


    Jeshi la polisi linaumuhimu wa kurejesha maofisa wake kwenye mafunzo au wapatiwe refresher courses mara kwa mara ..KIZIBITI UNAKISHIKAJE NA MIKONO YAKO BILA GLOVES ....SASA FINGER PRINTS SI ZITAKUWA ZA ASKARI mmhhhhhh

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 26, 2013

    Wasi wasi wangu ni pale mtuhumiwa atakapoikana hiyo Bastola na Askari kanzu keshaipapasa bila hata gloves.

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 26, 2013

    Kaazi kweli kweli. Hiki kituko jamaa kapanda kwenye Boda boda kasimamishwa kakutwa na bastola. Polisi bila kuchunguza kama anaimiliki kihalali au laa! wanamdhalilisha kwa kupiga picha na kuweka kwenye vyombo vya habari. Ikibainika kama anamiliki kihalali jeshi la polisi litamuomba radhi? na kupanda pikipiki na kuwa na Bastola ni kosa siku hizi? Kwa kuwa majambazi wengi wanatumia bodaboda basi wote wanaopanda usafiri huo na kuwa na Bastola ni wahalifu?
    Kwa kweli inanistaajabisha na jamaa akiwa ana miliki kihalali hawaoni watakuwa wamesha hatarisha usalama wake kwa kuweka wazi aina ya silaha anayomiliki?
    Jeshi letu la POLISI halifundishwi privacy? siyo kila jambo ni la kuweka hadharani wakati mwingine wanahatarisha usalama wa wananchi. Wana USALAMA wetu wasipende "CHEAP POPULARITY AT THE EXPENSE OF DAMN INNOCENT CITIZEN" siungi mkono UHALIFU NA WAHALIFU bali napenda Polisi izingatie privacy ya raia wema wanakimbilia piga picha akiwa ana miliki kihalali je? Wanataka vyeo kwa kuonekana wanafanya kazi?

    Kingine inakuwaje KIZIBITI kinashikwa hivyo na polisi tena pasipo hata kuwa na gloves akimruka kuwa ni yake atafanyeje maana kama imetoka kwenye kufanya UHALIFU hicho kitakuwa kimbembe chake anashikaje kizibiti bila hata protective gear jamani? Hawa polisi wetu wanafundishwa kweli? angalia alivyoshika kama MAANDAZI hahahahah!

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 26, 2013

    Usanii mtupu. Hapo police wamepata mlo wa leo. Rafiki yangu ana supermarket, pia ana camera dukani. Alipoibiwa kawashika wezi na ushahidi ni ule mkanda. Kawapeleka kawe police. Walilala siku 2 tu, walipopata fedha ya kuwapa police wakatolewa na mkanda ukapotea. Chezea police ya bongo wewe!

    ReplyDelete
  25. AnonymousJune 26, 2013

    Napenda sana namna polisi wanavyoendesha shuhuli zao nchini. Askari anapakatia ushahidi namna ile peku peku hakuna haja ya kuhifadhi alama za vidole kwenye bastola hizo kwa sababu watakalo sema kortini hakimu atawaamini. watuhumiwa wako free na hata hawana wasi wasi na wanacheka ingawa wanatuhumiwa kukutwa na silaha hatari sana. Na mwisho ingwawa watuhumiwa wamekutwa na chombo chenye kuweza kusababisha kifo hakuna kurusha rungu lakini subiri kwenye mkusanyiko wa watu huko ni rungu ni rukhsa.

    Tanzania tambarareeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  26. AnonymousJune 26, 2013

    Anony hapo juu muongo sana, Ukikamatwa Ulaya unapewa haki ya kupiga simu 3 kila baada ya muda fulani. kati ya hizo simu 3 ni ya wakili na kama hauna wakili unatafutiwa. Na kama hauna wakili una haki ya kutokubari kuojiwa bila ya kuwa na wakili ktk hayo maojiano.

    ReplyDelete
  27. AnonymousJune 26, 2013

    Good job askari wetu, angalau tuwape sifa. Lakini hicho kidhibiti kinashikwa na na polisi bila gloves wala nini, yaani bare hands like that? Sasa finger prints zinakuwa za kwao tayari ushahidi umeshapotea.. Askari wetu inabidi wafuate professionalism katika kukamata watuhumiwa na vidhibiti na kuhakikisha hawaharibu ushahidi baada ya kufanya kazi kubwa yote hiyo..Japo is too early to judge, kama ni kweli hali hii inaogopesha kwani hawa Watuhumiwa huwezi kudhania kuwa wanaweza kuwa majambazi au kubeba bastola..

    ReplyDelete
  28. AnonymousJune 26, 2013

    Je anaimiliki kihalali????????????

    Halafu na wewe mdau wa Ughaibuni??? ni ughaibu gani huo wa kumuweka mtu siku tatu bila mawasiliano? au Manzese hiyo?

    ReplyDelete
  29. AnonymousJune 26, 2013

    Hakuna ughaibuni ambako mtuhumiwa harusiwi kuwasiliana na jamaa zake au wakili.Hapo mdau umechemsha na umedanganya.Omba msamaha kwa wadau kwani haya mambo ya ughaibuni ulikuwa huyajui vema.

    Mnadhani gloves ndo zinasaidia sana hadi mkalaumu watu kushika bunduki bila gloves!Kinachojaliwa sana ni record ya bunduki,je mmiliki ni yeye?Yaani aliyeshikwa nayo ndiye mmiliki.Kama siye gloves za nini.Gloves zinatumika sana kama bunduki imekutwa kwenye tukio au la mapigano ama mauaji lakini haiku mikononi mwa mtu.

    Lakini pia cha msingi ni kile alichosema mdau kuwa ngoja kwanza tuwasikilize polisi na uchunguzi wao.Tusihukumu tu.Maana mahakimu wa mitaani tuko wengi.Kukutwa tu na bunduki si neon,labda ndiye mmiliki,au naye yupo kazini ila tu hawa waliomkamata hawajuani naye bado.

    Nakumbuka kisa kilitokea siku moja tulikuwa kwenye basi la Buguruni Posta,abiria mmoja alikuwa na pisto kiunoni,ilionekana na abiria mwingine kwa kuwa mmiliki alikuwa ameshikilia bomba hivyo shati lake limeinuka juu.Abiria wakabonyezana hadi kumweleza dereza ambaye naye akachepuka na gari kuingia kituo cha polisi.Konda ghafla akawaita polisi ndani ya basi kuna mtu anabunduki pisto.Mara yule jamaa akakamatwa kutiwa kituoni.Katoa kitambulisho kumbe ni afisa wa usalama jeshini alikuwa kazini.

    ReplyDelete
  30. AnonymousJune 26, 2013

    Yaani huyo askari kwenye picha ya kwanza kabisa ndio kafurahisha jamii!! unakamata bastola na index finger kwenye trigger on a loaded gun??? usalama uko wapi hapo??? du kweli umechemsha!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...