SIKU moja baada ya Simba kumalizana na mchezaji wake Amri Kiemba (pichani), mchezaji huyo sasa yupo sokoni na atauzwa kwenye timu ya Wydad Casablanca ya Morocco. Kiemba alimwaga wino wa kuichezea Simba kwa miaka miwili jana kwa dau la Sh35 milioni huku atakuwa akikunja mfukoni kitita cha Sh2 milioni kama mshara wake. 
 Awali mchezaji huyo alikuwa akiwaniwa na mahasimu wao Yanga, na Simba ingezubaa basi kiungo huyo angerejea nyumbani kwa mabingwa hao wa Tanzania bara. Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano Zakaria Hanspope tayari ametua Morocco akitokea Tunisia ambako alikwenda kufatilia fedha zao za usajili wa mshambuliaji wao Emanuel Okwi anayekipiga kweney timu ya Etoile du Sahel nchini Tunisia. 
 Okwi alijiunga na timu hiyo ya Tunisia mapema mwaka huu baada ya Simba kumuuza kwa dola 300,000 lakini klabu hiyo ya Etoile Du Sahel imekuwa ikizingua kulipa fedha hizo. 
 Lakini jana Hanspope alisema "Nimeshatoka Tunisia nipo Moroco na nimeshafanya mazungumzo ya awali na viongozi wa Wydad Casablanca n kesho tunafanya mazungumzo ya mwisho kabla sijarejea Dar, kila kitu kinaenda vizuri, naamini tutafikia mwisho mzuri." 
 Simba waliingia mchecheto wa kumsajili mchezaji huyo baada ya kutonywa na kigogo mmoja wa TFF ambaye pia ni mnazi mkubwa wa Simba kuhusu timu hiyo kuvutiwa na Kiemba na kushauri asajiliwe haraka ili Simba wapate faida kwa kumuuza. 
 Casablanca walimuona mchezaji huyo wakati wa mchezo kati ya Stars na Morocco ambapo Stars ililala kwa mabao 2-1 goli ambalo la ni kufutia machozi lilifungwa na Kiemba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2013

    Ukisikia mpira wa Bongo unakwenda ki Simba na Yanga ndio hivyo. TFF hakuna professinalism yeyote na hapo ni hakika atakula commission kwani alijuwa kuna ulaji ndio akawaambia Simba wamsajili haraka lakini si kwa manufaa ya mpira wa Tanzania. Ulafiii.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 13, 2013

    Anonymous maneno yako kisu maana sina hata la kuongeza bali kusema swadakta bro....

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...