Mkuu wa kitengo cha Vipaji na Uendelezaji wa Biashara kutoka  ROCKSTAR4000,Christine “Seven” Mosha , akifafanua jambo mbele ya Wanahabari kwenye mkutano wao uliofanyika jijini Dar kuhusiana na Kundi la kipaji cha televisheni “Orijino Komedi”  kuingia mkataba na Kampuni ya Nexus Consulting Agency kwa  kushirikiana na Rockstar 4000.
 Pichani shotoni ni Mpoki akizungumza machache kwenye mkutano huo, kati ni Joti na  Mkurugenzi mkuu wa Nexus, Bwana Bobby Bharwani
 kutoka kushoto ni Mpoki, Joti, Bobby, Seven, Seki, Masanja na Maclegan
Mpoki, Kitenge, Maulid, Joti, Seki, Masanja na Maclegan

=========== ====================

KUNDI LA KIPAJI CHA TELEVISHENI KINACHOONGOZA TANZANIA 
 ORIJINO KOMEDI WASAINI MKATABA MNONO WA USIMAMIZI 

Kundi la kipaji cha televisheni “Orijino Komedi” linaloongoza nchini kwa vipindi vyake  kupitia television imeingia mkataba na Kampuni ya Nexus Consulting Agency kwa  kushirikiana na Rockstar 4000. Mkataba huu unakuwa wa kwanza kwa wasanii wa  luninga kupitia kampuni hii ya Nexus

Nexus imenunua haki zote za usimamizi wa biashara na uongozi wa kundi hilo ambalo  linajulikana sana nchini kupitia vichekesho vyake kupitia vituo vya televisheni na  matamasha mbali mbali ambapo mkataba huu utakuwa ni kwa ajili ya kusimamia kipindi  hiki cha vichekesho kinachoundwa na wachekeshaji saba wajulikanao kama; Joti,  Maclegan, Masanja, Wakuvanga, Mpoki, Vengu na David Seki ambacho kimekuwepo  hewani kwa mfululizo wa miaka sita.

 Kushirikiana na Orijino Komedi ni kitu cha muhimu kwa Nexus kwani siku zote  imekuwa ikitamani kufanya kazi kwa karibu na kundi hilo na kuthamini kazi zao  kutokana na vipaji vya hali ya juu walivyokuwa wakionyesha wasanii wa kundi hilo;  alisema Mkurugenzi mkuu wa Nexus, Bwana Bobby Bharwani. 

“Nimefurahishwa sana kufanya kazi na watu wenye vipaji vya hali ya juu na kuiingia  mkataba na Kampuni ya Nexus Agency. Kwa pamoja tumedhamiria kukuza na  kubadilisha dhama ya vipaji na sanaa kutoka ilipo na kuwa ya kimataifa” alisema  Christine “Seven” Mosha , Mkuu wa kitengo cha Vipaji na Uendelezaji wa Biashara kutoka  ROCKSTAR4000.

Muandaji wa vipindi vya Orijino Komedi, Sekioni Davis ‘Seki’ amesema wanafuraha  kuingia mkataba wa kazi na kampuni ya Nexus Agency na Rockstar 4000 Africa, mbapo ameahidi kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanafikia malengo yao ya kukidhi haja ya soko.

Kwa kushirikiana na Rockstar 4000, nexus inatambua na kuthamini vipaji hivyo  itahakikisha inaendeleza vipaji vya wasanii wa kundi hilo ili vipaji vyao viweze kufikia  kiwango cha juu vya ufanisi ndani ya Afrika na kimataifa kwa ujumla. 

Jiunge na kufuatilie Orijino Komedi kwenye:
Website 
www.orijinokomedi.com
YouTube
www.youtube.com/orijinokomedi
Twitter
www.twitter.com/orijinokomedi
Facebook

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. hawa jamaa ni kwishney hawana tena lolote na nawashauri sasa waje tena kiupya kwani hata watoto hawaangalii tena vipindi vyao

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 13, 2013

    Mbona vengu na wakuvanga hawapo? Au wamewatupa ili msosi uwe mwingi kwao hawa jamaa? Acha uchoyo. vinginevyo hatuangalii tena.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 13, 2013

    HAPAN, WANATAKIWA TU KUWA WABUNIFU NA PIA KUANGALIA WENZAO NJE WANAFANYA NINI. BE CREATIVE NA KUJIUPGRADE

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 13, 2013

    Ni kweli kabisa, jaribuni kwenda na wakati. Chekesha at the same time fundisha! Watu sasa wanangalia ile comedy ya Star TV. Ipo juu ile mbaya! Unacheka na unapata somo.
    Kwavile mlishajijengea jina basi ushauri wangu ni huo, fanyeni mageuzi ya khali ya juu na haraka iwezekanavyo ili mlete kitu tofauti. Kama alivyosema mdau aliyetangulia, hakuna mtu anayewangalia kwa sasa.All the best! We love you!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...