Mwanamuziki Jady Jay Dee akionyesha umahiri wake wa kulishambilia jukwaa wakati wa show yake ya kutimiza miaka 13 katika Muziki iliyofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Nyumbani Lounge,Namanga jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wadau mbali mbali.
Ilikuwa ni shangwe tupu wakati wa show hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Mh. Joseph Mbilinyi akiwa stejini kutoa burudani mbele ya Mashabiki Lukuki waliofika Nyumbani Lounge kuona show ya Miaka 13 wa Mwanamuziki Lady Jay Dee.

KUONA PICHA ZAIDI



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 15, 2013

    Mwanamume yeyote aliyekamilika kiakili(gentleman) hawezi kushindana/kugombana na mtoto wa kike(mwanamke) hadharani!

    Tena inakuwa mbaya pale unapoamua kutumia chombo cha habari katika kutimiza haja yako!

    Na inakuwa mbaya zaidi kama ikitokea utakuwa na mamlaka nacho na hicho cha habari!

    Kwasababu hii itakuja kuathiri hata wengine ambao hawahusiki, kitu ambacho kinaweza kuwagawa watu katika jamii, na pia hata wafanyakazi wote katika tasnia yote ya vyombo vya habari wanaweza kugawanyika kwasababu tu ya ujinga au chuki za mtu mmoja dhidi ya mtu flani.

    Kitu cha kukumbuka hasa hasa kwa sisi wanaume, mwanamke ni kiumbe dhaifu ukimwangalia kwa nje kwa haraka haraka, lakini ukimwangalia kwa makini ni kiumbe mwenye nguvu ya ajabu kwa ndani!

    Mwanamke ananguvu ambazo hazionekani kwa macho, ila zinaoneka kwa ushawishi na mvuto wake katika jamii yoyote inayomzunguka! Na hizi nguvu zinakuwa ni za hatari sana pale inapotokea wanawake wenzake wote wanaomzunguka wakamsapoti!

    Kwahiyo kitu cha kukumbuka ni kwamba (sisi wanaume), huwezi kutumia chombo chochote cha mamlaka katika kushindana na mwanamke hasa hasa hadharani!

    Kama kunasehemu mtu amejikwaa kwa kujua au kutojua, inabidi hajisahihishe kiutuuzima, lasivyo jamii nzima inaweza kumdharau!

    Na usipokuwa makini hata wale wote wanaomzunguka katika maisha yake ya kila siku wanaweza wakamshusha thamani na kumkosea heshima kwa njia moja au nyingine!

    DON'T FIGHT/QUARREL WITH WOMAN IN PUBLIC, BECAUSE SHE HAS GREATER CHANCE OF 100% OF PROOFING YOU WRONG IN ALL ASPECTS!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 16, 2013

    VIVA JIDE watakoma kuringa na Radio yao hiyo ya UKANDAMIZAJI wa WASANII. Sisi tunasonga mbele !!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 16, 2013

    Well said mdau...

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 16, 2013

    Nadhani ujumbe umefika.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 16, 2013

    tupe na MWANA FA pia, ilitisha sana na ilitulia.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 17, 2013

    2cpende kushabikia v2 2cvyojua kwanza mwana fa kiingilio 50,000 huy jdee 10,000 wap na wap jaman?! Mwana fa Yuko mbali sana halaf ilkuwa show ya kstaarab cyo huko nymbn longe kujambiana2 utafkr taarab

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...