Pichani ni Daraja la Mto Wami Mkoani Pwani ambapo kuna moja ya vyanzo vikuu vya Maji hapa nchini.
Huu ndio Upana halisi wa Daraja la Mto Wami ambalo haliwezi pitisha gari zaidi ya moja.
Kitu cha Air Force One kikipandisha mliwa wa Wami.
Malori na Mabasi katika kona za Milima ya Wami.
Huu ndio Mto Wami wenyewe.
Kuzuri kweli kweli, ila ukikosea njia tu mamba wanakusubiri huko kwenye mto.
ReplyDelete
ReplyDeleteNadhani humo ndani ya Air Force One yumo Obama
Mmmh, hata sina la kusema, hivi inakuaje watu wanaamua kutumia hela kujenga daraja la namna hiyo aisee, watu wengine wanafaa kuchapwa vibao, daraja linapitisha gari moja tu kwa wakati mmoja, hai ingii akilini. Halafu ajali zikitokea hasa usiku, maana taa zenyewe za barabarani hamna, mara barabara ghafla inabadilika inakuwa nyembamba darajani. Hpana kwakweli, inabidi hiyo barabara ipanuliwe yapite magari mawili ajali nyingine huwa zinazuilika.
ReplyDeleteWahusika wasafishe Daraja na barabara. Wa karabati kuliko bomolewa kwa ajali au makusudi; waweke taa hasa kwa sababu mkondo ni mmoja tu kupita gari kisha waongeze Daraja lingine kama hilo ili iwe njia Mbili. Hili Linawezekana kutokana na Utajiri wa Tanzania ilihali viongozi wakiwa na Busara.
ReplyDeleteSALAAM, NDUGU WANANCHI KWA UJUMLA. MIMI NIMEGUSWA SANA NA PICHA ZOTE NA MAONI YA WALONITANGULIA, NILIWAHI TOA MCHANGO WA MAWAZO KUHUSIANA NA AJALI ZA MTO WAMI, KWAKO MICHUZI LKN KWA BAHATI MBAYA HUKUTOA MAONI YANGU. KWA KWELI HAPA YANATAKIWA MADARAJA 2 YAANI MOJA LA KWENDA NA LINGINE LA KURUDI NA PIA YAWE YA KIWANGO CHA KUPITISHA MAGARI MAWILIMAWILI KWA KILA DARAJA. NCHI YETU INAWEZA FANYA HILI JAMBO HALISHINDIKANI LABDA TU VIONGOZI WAAMUE KUTOLIFANYIA KAZI SWALA HILI. MAANA NI KWA FAIDA YETU KAMA NCHI NA USALAMA WETU KISAFARI HUSUSANI ENEO HILI LA WAMI. NAOMBA WADAU WENYE UJUZI WASAIDIE KTK MAWAZO PIA
ReplyDelete