Katibu Mtendaji wa Asasi isiyo ya Kiserikali wilayani Kilwa,Omary Mkuwili akitoa maelezo mafupi kuhusiana na Mdahalo huo wa Uwajibikaji wa Viongozi wa Serikali za Mitaa Chini ya Ufadhili wa The Foundation na kufanyika jana katika Tarafa ya Pande wilayani Kilwa.
Baadhi ya wadau mbalimbali waliohudhuria Mdahalo Huo wakichangia mada

Na Abdulaziz Video,Kilwa

Wananchi wa kata ya Pande, wilayani Kilwa,mkoani Lindi wanakerwa na tabia ya mbunge wao wa Jimbo la Kilwa Kusini, Selemani Bungala Bwege ya kukwepa kushiriki kwenye vikao vya Bunge la Jamhuri la muungano kwa muda Mwingi na hasa bunge la bajeti.

Wakizungumza kwenye mdahalo Unaohusu uwazi na uwajibikaji wa Viongozi na watendaji wa serikali za mitaa kwa maendeleo ya wananchi ulioandaliwa na Mtandao wa mashirika yasiyo ya kiserikali wilaya ya Kilwa,(KINGONET) kwa ufadhili wa The foundation for civil socitey na kufanyika katika shule ya Msingi ya Pande, wananchi hao, Akiwemo Bw Anan Nahoda, Saidi Athumani Kifuku na Mariamu Kajoka walisema kuwa muda wote wa kipindi cha mikutano ya bunge huko Dodoma mbunge huyo uwa hanaonekana mitaani akifanya mikutano ya kuhamamsisha wananchi wagomee malipo ya pili ya korosho badala ya kuwa bungeni.

Anan Nahoda mkazi wa Pande alisema kuwa,kitendo cha Mbunge wao kukwepa vikao vya bunge vinawaumiza kwani moja kati ya kazi ya mbunge ni kuwakilisha mawazo ya wananchi kwenye mikutano ya bunge na kitendo cha mbunge wao kutokuwepo huko inaonyesha hatimizi wajibu wake ambao wapiga kura walimchagua hawatekelezewi.

“Kinachotusikitisha sisi tuliomchagua ni kumwona mbunge wetu muda wote wa bunge yupo nje ya bunge tena kama kuondoka ni leo kwani hata jana alikuwepo hii inafanya tusiwe na mwakilishi kule bungeni hii si halali kwani hata akiwepo huku hashughuliki na masuala ya maendeleo badala yake anaendesha mikutano ya ndani ya kushawishi wananchi wagomee malipo ya korosho”alisema Anan.

Aidha Anan alilalamikia tabia ya mbunge huyo kutotembelea na kutofanya mikutano na wananchi ili kukusanya kero na maoni mbalimbali na kuyasemea akiwa bungeni na kudai kuwa tangu achaguliwa hajafanya mkutano wowote wa hadhara unaojumuhisha wananchi licha ya kufanya mikutano ya ndani.

Saidi Athuman alisema kuwa, tatizo la viongozi wengi waliochaguliwa ni kutofahamu vyema mfumo wa vyama vingi kwani badala ya kushughulikia matatizo ya wananchi hujikuta wakishughulikia maslahi ya vyama vyao vilivyowawezesha kuwa madarakani hali ambayo inarudisha nyuma maendeleo ya nchi na kusababisha uvunjifu wa amani na kuwataka wajue majukumu yao kwa wananchi waliowachagua.

Kufuatia malalamiko hayo,Mtandao ulimtafuta Mbunge Huyo kwa njia ya Simu ili kutoa ufafanuzi wa tuhuma hizo Ambapo Bungala alikanusha tuhuma za kutofanya mikutano kwenye kijiji na kubainisha kuwa tangu amechaguliwa amefanya mikutano saba ambapo alikutana na wananchi mbalimbali kupokea kero zao,na kuhusu la kutohudhuria bunge alikiri kutokwepa vikao vya bunge na kuwa hivi karibuni alionekana jimboni kwake na kudai kuwa alikuwa kwenye shughuli za uchaguzi ndogo ulizofanyika hivi karibuni wilayani Nachingwea ambapo alikwenda ili kusaidiana na viongozi wenzake kumnadi mgombea wa chama chake(CUF).

“Ni kweli sikuwepo kwani nilikuwa kwenye kampeni ya uchaguzi mdogo huku Nachingwea ili kuhakikisha mgombea wetu anashinda na sasa hivi naelekea bungeni….hoja ya kutoonekana muda mwingi bungeni hiyo si kweli na ili la kutofanya mikutano si kweli labda huyo aliyelalamika hakuwepo…. kwani nimefanya mikutano mingi hapo na wa mwisho ni wa mwezi wa pili mwaka huu”alisema Bungala.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 25, 2013

    Huyo anayelalamika naona ana maslahi binafsi.Huyu mbunge Bwege anajitahidi sana kuhakikisha wananchi wa kilwa wanapata haki yao. Mfano zao la ufuta, aliacha vikao vya bunge kuhakikisha wananchi wanapata maslahi yao kwenye ufuta. Alichofanya ni kuwaeleza watendaji wa serikali kwamba ununuzi wa ufuta uwe huru kwa kila anayetaka kununua ufuta, lakini bei iwe angalau iwe ile iliyowekwa na serikali, yani kima cha chini.

    Kulikuwa na kubishana sana na wale wanaotaka stakabadhi ghalani, lakini mbunge alihakikisha haki inatendeka kwa wakulima. Matokeo yakawa mazuri, wanunuzi wakanunua ufuta kwa sh 1,600 kwa kilo badala ya sh 1,400 kwa kilo.

    Ilulu ndiyo wanataka stakabadhi ghalani, na bei yao waliiweka sh 1,400. Hawakupata hata kilo moja. Na moja ya mfumo wa stakabadhi ghalani ni kwamba unalipwa nusu au kiasi kingine chochote nyingine baadae. Maana yake ni kwamba kama Ilulu ndiye angekuwa ni mnunuzi pekee wakulima wangeuza kwa sh 1,400 kwa kilo, na wasingepewa yote. Wangepewa nusu au kiasi kingine chochote na inayobakia ni siku nyingine. Nadhani kila mmoja amesikia matatizo ya stakabadhi ghalani (Ilulu) katika wilaya ya Liwale, Ruangwa, na Nachingwea.

    Kwa hiyo mbunge Bwege anastahiki kwa kuwawezesha wakulima kuuza ufuta kwa sh 1,600 na kulipwa yote kwa pamoja bila mkopo. Ndiyo maana hujasikia malalamiko kutoka kwa wananchi wa kilwa kuhusu zao la ufuta kama ilivyo kwa wenzao wa liwale, nachingwea, na ruangwa.

    Wabunge wa namna hii wanahitaji sapoti kubwa toka kwa wananchi ili waendelee kusimamia maslahi ya wananchi kwa maslahi ya nchi.

    Muumba ajaalie kheri kwa wananchi na nchi kwa ujumla, na ampatie afya njema na mwisho mwema mbunge Bwege. Aendelee kusimamia maslahi ya wananchi kwa maslahi ya nchi, Muumba amsaidie.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 25, 2013

    Haya majina yana athari kubwa katika maisha ya binadamu we mwite mtoto Shida kila siktu shida mwite Tabu kila siku tabu haya jina la mbunge Bwege na nyie wananchi bado mnachagua bwege liwaongoze sasa mnalalamika nini si mlimchagua wenyewe.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 25, 2013

    Jamani kwani jina linafanya kazi? Kwani mtu kuitwa Bwege ina maana hawezi kufanya kazi? Kuna wangapi wana majina mazuri hawahudhurii bungeni wala kuitisha mikutano kwenye majimbo yao? Tuweni na weledi ktk kutoa mawazo yetu. By mdau

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...