Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk (wakatikati)akisikiliza maelezo kutoka kwa Fundi Mkuu wa Zbc Radio Ali Aboud alievaa kanzu kushoto kutokana na kuunguwa kwa Kifaa cha Waya wa Cable na kusababisha Radio kutokusema kwa siku kadhaa kwa kutumia masafa ya Kati (Midium Wave) hapo katika kituo cha kurushia matangazo Bungi Wilaya ya Kati Unguja.
Mhandisi wa Kichina Zhao Wei Min akitoa ufafanuzi wa Kifaa cha Waya wa Cable kilichoungua na kusababisha Radio kutokusema kwa siku kadhaa kwa kutumia masafa ya Kati (Midium Wave)mbele ya Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk alipofanya ziara makusudi ya kuangalia matatizo hapo katika kituo cha kurushia matangazo Bungi Wilaya ya Kati Unguja.
Waziri wa Habari Utamaduni Utalii na Michezo Said Ali Mbarouk wakwanza kulia akitoa maelekezo kwa wafanyakazi kuhusu namna ya kutatua tatizo la kuungua kwa Kifaa cha waya wa Cable ambacho kimesababisha Radio kutokusema kwa siku kadhaa kwa kutumia masafa ya Kati (Midium Wave) hapo katika kituo cha kurushia matangazo Bungi Wilaya ya Kati Unguja. PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 07, 2013

    kwenye ziara ya kikazi waziri hapaswi kuvaa hovyo namna hiyo. hilo shati alilovaa mheshimiwa waziri linapaswa kuchomekewa wakati wote. hata kanzu nayo iwe na maelekezo ni kanzu ya aina gani ili mhusika aonekane amevaa kanzu lakini yuko profesional.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 07, 2013

    We, acha u-fashenita usiojua!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 07, 2013

    Hapo kweli ila, mdau nadhani ungeshangaa zaidi kama tungeoneshwa mguuni kavaa nini?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 07, 2013

    Nakuunga mkono, wavae vizuri na waonekane professional, kama "mchina" alivyovaa vile.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 08, 2013

    Kweli nilitaka kuandika kuhusu professionalism. Anon wa hapo umeshatoa maelezo ya kutosha.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 08, 2013

    Wadau naomba msaada. Katika picha hiyo waziri ni yupi?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 08, 2013

    Ndio maana tunataka serikali yetu ili tusiwabughudhi kwa mavazi yetu, kwa akili zako wewe mchangiaji wa kwanza vazi ni bora kuliko ithibati, ari, ukweli na mapenzi ya uongozi?? Hao wanaokufurahisha kwa kuvaa suti ndio hao hao wanaokwiba na kufisha nje huku wengine wakitorosha mchana kweupe.Acha ushamba wewe.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 08, 2013

    Ukisema Mhandisi wa Kichina kidogo kama inaleta maana ya Mhandisi feki hivi. Nadhani ingeandikwa Mhandisi kutoka China ingeleta maana nzuri zaidi. #MaoniYangu

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 08, 2013

    Sijaona ubora wa mavazi ya huyo mchina zaidi ya kutu kwenye macho na mawazo yenu!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 08, 2013

    Besides the mavazi in which I didnot envy the way dressed.What is the solution to the occured problem.Is the kifaa fixed or not.It looks like a lot of porojo going on !!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...