Basi la abiria mali ya Kampuni ya Safari, lenye Nambari za Usajili T 9957 BZT likiwa limelala ubavu baada ya Dereva wake kushindwa maarifa wakati akikata kona kali, katika Kijiji cha Ngumbalu, Wilayani Namtumbo Mkoani Ruvuma.Katika ajali hiyo ni Dereva peke yake ndie alieumia na kufanikiwa kukimbizwa Hospitali kwa Matibabu
Askari Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani akiangalia namna Basi hilo kilivyoharibika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 17, 2013

    Pole walio umia
    Lakini tutazidi kusikia mikasa ya ajali kama hizi. Kwani sehemu nyingine za hizi barabara ni mitego ya panya.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 17, 2013

    Ndugu zanguni, hiyo barabara imewekwa lami kutusaidia na adha ya usafiri haswa wakati wa mvua, chonde chonde spidi bila maarifa hazifai, tutageuza barabara kuwa chinja chinja badala ya changamoto ya maendeleo.
    ombi langu kwa watu wa Songea, Namabengo, Namtumbo hadi Tunduru, barabara itakapo kamilika basi tuitumie kwa busara ilete maendeleo na sio majanga kwa raia wasio na hatia!
    Hongereni kwa hatua katika maendeleo ya kusini mwa Tanzania, naiona Mtwara corridor inakuja na neema kwa wantanzania!

    Mungu ibariki Tanzania!

    Mdau,
    Mwenge, D'salaam

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 17, 2013

    Poleni sana wote mliopatwa na mkasa huu. Mwandishi basi hili limepinduka, kupiga mwereka ni kama kufanyia mzaha au kejeli ! Div 0

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 17, 2013

    inawezekana kuna uzembe,ila ni vizuri barabara ziwe na alama kama vile kona na pia kiasi cha mwendo kasi dereva anachotakiwa kuendesha,barabara nyingi sana ama hazina alama au alama zinatolewa hatua chache kabla ya eneo husika, mfano vibao vya matuta,mwendo kasi, kona au hata matengenezo yanayoendelea mbele.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...