Benki ya Dunia imetoa changamoto kwa nchi
za Afrika kuhimiza maendeleo endelevu ya ardhi ili
kupunguza umaskini na kujiletea maendeleo.
Ripoti ya Benki hiyo iliyotolewa Julai 22, 2013 imeeleza
kuwa ingawa nchi za Afrika ina karibu nusu ya eneo la ardhi nzuri
ambayo haijaendelezwa kwa kilimo, bara hilo limeshindwa kuiendeleza
ardhi hiyoinayokadiriwa kuwa hekta milioni 202 kujikwamua katika umaskini,
kuleta maendeleo ya uchumi,kuongeza nafasi za kazi na kulleta mafanikio
kwa jumla.
Ripoti hiyo inayoitwa “Kutumia
ardhi ya Afrika kwa mafanikio ya pamoja,” inaeleza kuwa
nchi za Afrika najamii zake zinaweza kabisa kuondoa tatizo la uporaji
wa ardhi, kuzalisha mazao ya chakula na kubadilisha taratibu za
usimamizi na umiliki wa ardhi katika mwongo ujao.Afrika,
Ripoti hiyo imeeleza, ina kiwango
kikukbwa cha umaskini ambapo asilimia 47.5 ya watu wake wana kipato
chini ya dola za Marekani $1.25 kwa siku..
“Licha ya kuwa na ardhi kubwa na utajiri wa madini, Afrika bado ni maskini
,” anasema Makhtar Diop, Makamu wa
Rais wa Benki ya Dunia kwa Afrika.
“Kuboresha usimamiaji wa ardhi
ni muhimu kwa maendeleo ya haraka na kutoa nafasi zaidi kwa waafrika
, wakiwemo wanawake ambao ni asilimia 70 ya wakulima wa Afrika ambao
wanakwazwa kumiliki ardhi na sheria za kimila..Hali hii haikubaliki na lazima
ibadilike ili waafrika waweze kunufaika na ardhi yao.”
Ripoti hiyo imeeleza kuwa zaidi ya asilimia 90 ya ardhi ya ardhi haijarasimishwa,
hivyo kuwa na hatari kubwa ya uporaji na kuchukuliwa kwa malipo ya chini
ya fidia.
Hata hivyo kumekuwa na matumaini
ya maboresho chini ya mipango inayoendelezwa katika nchi za
Ghana, Malawi, Msumbiji,, Tanzania, na Uganda ambapo mpango wa
kutumia ardhi kwa mafanikio ya pamoja unaweza kuleta mapinduzi
ya uzalishaji wa kilimo na uporaji wa ardhi na kuondoa umaskini
wa kutupea Afrika..
Mpango wa kuleta mabadiliko
Ripoti hiyo inapendekeza kuwa Afrika inaweza kufanikiwa kuendeleza ardhi
yake katika kipindi cha muongo ujao kwa::
· Kuwa na mabadiliko na uwekezaji
kurasimisha ardhi na maeneo muhimu yanayomilikiwa na watu
binafsi.
· Kusimamia taratibu za umiliki za
maeneo yaliyovamiwa na kujengwa bila mpangilio mijini ambapo
wanaishi zaidi ya watu asilimila 60 barani Afrika. .
· Kukabiliana na udhaifu wa utawala
na rushwa katika mfumo wa usimamizi wa ardhi katika nchi za Afrika
ambao kwa kawaida unapendelea wakubwa na kuathiri maslahi ya wananchi
walio maskini.
· Serikali za Afrika kuwa na dhamira
ya kisiasa kuhimiza mabadiliko haya ya ardhi kuvutia raslimali
na uwezekezaji wa jamii ya kimataifa. .
Ripoti hiyo inasema kuwa mpango huo utagharimu nchi za Afrika
na washirika wa maendeleo , ikiwemo sekta bianfsi kiasi cha
dola za Marekani bilioni 4.5 katika kipindi cha miaka 10 kuleta
mabadiliko ya sera na uwekezaji
imetulia
ReplyDeleteSasa leo hii Mashamba ya Ukoo kule Vijijini watu wanawauzi wakwekezaji halafu wao wakipata fedha wananunulia magari na kujenge Majumba Mijini.
ReplyDeleteWorld Bank imesasambua ukweli wa Umasikini wetu ni kushindwa kuitumia ardhi yetu inavyostahili!
Hivi kweli suluhisho la ugumu wa maisha ni kuuza shamba au ardhi ya Ukoo huko Kijijini?
Haitoshi umeuza ardhi ama shamba, fedha tena huwekezi kwenye Mipango endelevu umeona kununua mgari na ujenzi wa Majumba ndio tija?
JIFUNZENI HOW TO DETERMINE ASSET CLASSES:
ASSETS:
-Shamba
-Ardhi
-Msitu
-Mashine ya kuchambulia mazao au ya ku-process madini
-Nyumba ya Kibiashara
NON ASSETS:
-Gari
-Simu kubwa huku mipango hakuna
-Nguo nyingi za bei ghali bila malengo
-Ulevi na sifa (Ujiko)
-Ngono zembe
-Sherehe nyingi kupita kiasi
Tazameni Uingereza ule Ukoo wa Kifalme Jeuri ya fedha wanaipata kutokana na umiliki wa ardhi Karne kwa Makarne hadi hii leo.
Halafu tunaambiwa kuwa shamba unaweza kuliweka rehani ukakopa mapesa benki. Benki zenyewe za kigeni. Ni njia mojwapo ya mabenji ya kigeni kujipatia mashamba endapo utashindwa kuwalipa au kufilisika. Na mabenki yatachukua shamba na kumwuzia yeyote!
ReplyDeleteJifunzeni the agro-revolution ya Uingereza jinsi ilivyoondoa peasantry culture; tumeanza hapa na tutabaki walalahoi tusioweza kukimbilia mijini ili tuajiriwe viwandani, kama huko uingereza ya zamani!
Umesema kweli tupu mdau! Shida Wa-Tz wengi wako ktk hulka ya matumbuzi na kuonekana. Wengi hawa kerwi na ustawi wa kizazi kijacho nao ni pamoja na watunga sera wetu, viongozi wetu. Hii laana ya umaskini wa fikra na hulka ya maendeleo endelivu itafikisha taifa pabaya.
ReplyDelete