Mwenyekiti wa TALGWU,Bwa, Andrea Mwandimbile pichani akifafanua jambo mbele ya wanahabari (hawapo pichani} zaidi kuhusiana na maandamano hayo kumuondoa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo.

Chama cha wafanyakazi wilaya ya kilolo wamepanga kufanya mandamano ya kumuondoa mkuu wa wilaya ya kilolo,Mh. Gerald Guninita kwa madai kuwa anawanyanyasa na kuwadhalilisha watumishi wa umma.

Wakizungumza na wandishi wa habari mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi wilaya ya kilolo TALGWU,Bwa, Andrea Mwandimbile, wamesema kuwa hawamwitaji mkuu huyo wa wilaya kutokana na utendaji wake wa kazi kwa wafanyakazi wa umma, kuwa wa vitisho.

Wamesema kuwa kutokana na kutoa kauli za vitisho kwa watumishi hao wa umma, zimekuwa zikiathiri utendaji na uhusiano makazini kutokana na wengi wao kufanya kazi kwa hofu.

Kwa upande wake katibu wa chama cha wafanyakazi wilaya ya kilolo TALGWU ,John Mbingi ,wamewataja watu ambao tayari wamefanyiwa udhalilishaji na mkuu huyo kuwa ni Thomas Nyambage, ambaye ni afisa mifugo na kaimu wao kata ya Mlafu pamoja na Beatus Nyato,Afisa usafirishaji kilolo ambao walipigwa pingu hadharani na kuwekwa ndani na kisha kuachiwa huru bila kufunguliwa mashitaka.

Aidha amesema tayari uongozi umeshafanya taratibu za kutoa taarifa kwa viongozi wa ngazi za juu akiwemo mkuu wa mkoa.kutokana na malalamiko hayo mkuu wa wilaya hiyo GERARD GUNINITA ambaye ndiye mlalamikiwa amekanusha mashitaka hayo na kusema kuwa hajapata malalamiko hayo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...