Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja ( suti nyeusi)akimkabidhi Zawadi ya Kikapu Kamishna Mkuu wa Magereza wa Zambia, Percy Chato. Kikapu hicho kimetengenezwa na Wafungwa wa Gereza Kuu Ukonga.  Hafla  fupi ya kuwakaribisha Wakuu wa Magereza Nchini toka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika imefanyikia katika Bustani ya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, Ukonga Dar es Salaam
 Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa hotuba fupi wakati wa hafla aliyowaandalia Makamishna Wakuu wa Magereza Nchini toka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika. Hafla hiyo imefanyikia katika Bustani ya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, Ukonga Dar es Salaam

  Mwakilishi wa Kamishna Mkuu wa Magereza Nchini Namibia, Bi. Feris akitoa neno la shukrani kwa Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, John Casmir Minja(Suti nyeusi)kwa kuwaandalia hafla hiyo fupi pamoja na kupata fursa ya kubadilishana mawazo ya namna ya Uendeshaji wa Magereza. Hafla hiyo imefanyikia katika Bustani ya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, Ukonga Dar es Salaam
 Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(Suti nyeusi) akiwa na Makamishna Wakuu wa Magereza kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika katika hafla fupi aliyowaandalia baada ya kumaliza Kikao cha Mawaziri wanaohusika na Ulinzi na Usalama toka Nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika( wa kwanza kushoto ni Kamishna Mkuu wa Magereza wa Zambia, Percy Chato, ( wa pili kushoto) ni Kamishna Mkuu wa Magereza wa Msumbiji, Dkt. Eduardo Sebastiao, (wa tatu kushoto) ni Kamishna Mkuu wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Tom Moyane, (wa kwanza kulia) ni Mwakilishi wa Kamishna Mkuu wa Malawi, Naibu Kamishna wa Magereza, Ms. Phiri, ( wa pili toka kulia) ni Mwakilishi wa Kamishna Mkuu wa Namibia, Kamishna wa Magereza, Ms. Feris. Hafla hiyo ilifanyikia katika Viwanja vya Bustani ya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, Ukonga, Dar es Salaam
 Kamishna Jenerali wa Magereza Nchini, John Casmir Minja(wa kwanza kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Makamishna Wakuu wa Magereza toka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika(Wote waliokaa), Wengine waliosimama ni Maafisa wa Jeshi la Magereza ambao wameongozana na Makamishna hao pamoja na baadhi ya Maafisa Waandamizi toka Makao Makuu ya Jeshi la Magereza . Hafla ya kuwakaribisha imefanyikia leo katika Bustani ya Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, Ukonga Dar es Salaam
Kikundi cha Sarakasi kinachoundwa na Askari wa Jeshi la Magereza wakionesha umahiri wao katika hafla ya kuwakaribisha kama unavyoweza kumuona Askari wa Kike ambaye alikonga nyoyo za Makamishna Wakuu wa Magereza toka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika.
Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...