Mabondia wa bigright boxing ya mwananyamala wapo kambini wakiendelea kujifua kwa ajili ya kuwakabili wapinzani wao ambao watazichapa nao katika wakati tofauti na maeneo mbalimbali hapa nchini na nje ya nchi.
Mabondia hao ni issa omar anaetarajiwa kuzipiga katika ukumbi wa Government complex nchini zambia na Pethias Chisonga wa Zambia chini ya uratibu wa Exodus Stable ya nchini humo. Hapa Dar es salaam Friends Corner hotel Mustafa Doto atazipiga na Rajab Mjeshi, Martin Richard na Mbena Rajab wao watakuwa mkoani Tanga huku Zumba Kukwe akizipiga Kibaha na mabondia waliobaki watamsidikiza Daudi Anthony’Odinga’ kuzipiga na Tom-po katika ukumbi wa Eagles pub Bagamoyo. Katika mapambano ya Bagamoyo yameratibiwa na Tan academy chini ya kiongozi wake Japhet Kaseba yatakuwa na ushindani mkali sana kwa wanafunzi watano wa Kaseba watakapozipiga na wanafunzi wa Bigright nje ya mkoa wao
Baadhi ya mabondia toka kambi ya Bigright boxing club wakiwa kambini kwenye gym yao Mwananyamala jijini Dar es salaam wakijiandaa kwa ajili ya mapambano yatakayofanyika siku ya idd.
mabondia wa bigright boxing wakiwa mazoezini katika gym yao iliyoko mwananyamala
Sparring ya nguvu
Big right Ibrahim kamwe akiwa na vijana wake gym
Tizi likiendelea
Vijana wakiwa tayari kwa mapambano
Hivi kwa nini mabondia wetu huwa wanfanya mazoezi kwenye mazingira duni na machafu?
ReplyDeleteLAKINI WANASHINDA PAMBANO KAMA YULE ALIEMCHAPA MTHAILAND AMBAE ANAFANYA MAZOEZI KWENYE MAZINGIRA MASAFI NIA TU KUIPENDA KAZI YAKO AMA MCHEZO WAKO NA KUJITUMA KWA UJUMLA.
ReplyDeleteASANTE
ni kweli mabondia wa Tanzania wapo katika mazingira mabovu kutokana na mchezo wenyewe kutojaliwa na wenye uwezo hivyo mabondia wanajiendesha wenyewe kama yatima
ReplyDelete