Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, (wa tano kutoka kushoto) akishiriki swala ya Magharibi na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu wa Mkoani Arusha, wakati wa hafla ya Futari ya pamoja aliyoiandaa na kufuturu na wananchi hao katika Hoteli ya Naura Mkoani Arusha jana Julai, 23, 2013.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwaongoza baadhi ya wananchi wa mkoani Arusha kuchukua futari, wakati wa hafla ya Futari ya pamoja aliyoiandaa na kufuturu na wananchi hao katika Hoteli ya Naura Mkoani Arusha jana Julai, 23, 2013.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na wageni wake baada ya kushiriki nao futari ya pamoja aliyoiandaa na kufuturu na wananchi hao katika Hoteli ya Naura Mkoani Arusha jana Julai, 23, 2013.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na mkewe Mama Zakia Bilal, wakiagana na wageni wao baada ya kushiriki nao futari ya pamoja aliyoiandaa na kufuturu na wananchi hao katika Hoteli ya Naura Mkoani Arusha jana Julai, 23, 2013. Picha na OMR.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 24, 2013

    Ankali plz muwe munacheki spellings kwanza jamanii. 'AFUTARU' au 'AFUTURU'? Hilo tu.. kazi nzur na blog nzur Tanzania nzima. Ramadhan Kareeem

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 24, 2013

    Hivi hii pesa ya kufuturisha kila mara wanavyofanya viongozi wa serikali ni pesa kutoka mifukoni mwao au kodi ya wananchi??

    Kama ni kodi ni nani amewapa mamlaka ya kutumia hizi kodi kwa mambo ambayo si ya serikali as serikal haina dini?

    Michuzi tafadhali usiibanie hii comment hata kama wewe upo serikaln..this needs to be explained maana si sahihi kutumia kodi kwa mambo binafsi yenye kupendelea dini moja!..je wakristo, wapagani,ect wakiamua kufuturishwa kwa sikuu zao nchi itakwenda hii??

    mdau
    new york

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 25, 2013

    Spot on mdau wa NY, I have had enough of these futaris kwa kutumia hela za wananchi. Tuelezeni wazi kama ni wao wanalipa au vipi?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 25, 2013

    Spot ON

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 25, 2013

    mdau new york hapo juu, udini tu ndio unaokusumbua,kwani watu wakikutana kwenye vikao hawanywi chai au lunch au diner???? kama ndivyo basi vp wakiamua kuahirisha hiyo lunch na ikaliwa jioni sababu wanakua wamefunga? mheshimiwa yuko kikazi,..wivu ni tu unakusumbua wewe!!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 25, 2013

    Hivi mke wa mhe. JINA ASHA AU ZAKIA?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 25, 2013

    Rukhsa nanyie kufuturishwa kwenye Kwarezma. Muhimu mfunge kweli tuu.

    Sijui ulishawahi kujiuliza pia pesa ya kupamba mapambo ya thamani kila aina kwenye ofisi za Serikali na kutuma zawadi za kadi na mivinyo kwenda kwa watu mbali mbali pesa hizo zinatoka wapi??
    Jiulize kote kote na utafakari pia.

    Serikali haina Dini ndio lakini watu wake wana Dini. Ni jukumu lake kuwatumika.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 25, 2013

    Jamani mimi ni muislam..lakini huyo mdau wa NY anapoint haijajibiwa kiutaratibu..swali lipo wazi..hajakataza kufurisha anachotaka kujua na mimi pia nahitaji kujua kuwa...viongozi hao wa serikali hizo futari wanalipia waumini na wanakaribisha viongozi kama wageni..au viongozi wenyewe wanatoa mifukoni mwao kama sadaka au serikali inalipa ili tujue bajeti ya kufurisha inatoka wapi...jamani tuwe wastaarabu tuhishimu dini za watu..

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 25, 2013

    mdau wa NY usishangae sana tz kila kitu kinakwenda kwa mazoea hata kama hayo mazoea ni kinyume cha sheria!

    Hushangai mtu anakamatwa na kosa then akiwa kituo cha polisi inapigwa simu kwa mkubwa na mkubwa anatoa amri aachiwe na anaachiwa maramoja!

    wenyewe wanaita "utaratibu tuliojiwekea"!!

    j4
    ujerumani

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...