Habari na Picha Na Dixon Busagaga
wa Globu ya Jamii Moshi. 
 WIZARA ya maji,imeelezea kutoridhishwa kwake na uendeshaji wa kampuni ya usambazaji maji wilayani Rombo ya Kiliwater kwamba haijajipanga kibiashara na ingeweza kupata faida kubwa kuliko hali waliyonayo sasa kama wangekuwa makini. 
 Naibu waziri wa maji Dk Binillith Mahenge alitoa kauli hiyo baada ya kupokea taarifa ya kampuni hiyo kuhusu usambazaji wa huduma za maji na mipango yao katika ununuzi wa mita kwa ajili ya kuwafungia wateja wao. 
 “Kwa mipango hii mliyonayo kama kampuni hii ingekuwa imekabidhiwa mfanyabiashara yeyote makini,angeshindwa kupata faida?” alihoji huku mwenyekiti wa bodi ya kampuni hiyo, Silayo akikiri kwamba faida ingepatikana. 
 Aliitaka kampuni hiyo kujipanga upya kwani wanayo fursa ya kupata faida kama wakijitahidi kupunguza maji yanayopotea lakini pia kuhakikisha wanaondokana na mfumo wa ulipaji anka kwa ‘Flat rate’ bali wawafungie wateja mita za maji. 
 “Huu mfumo wenu wa watu wote kulipa maji kwa viwango sawa unawapotezea mapato, wapo wanaoyatumia kwa ajili kumwagilia migomba kasha watalipa sh 3,000 kwa mwezi, ninyi mnaona hilo ni sahihi,badilikeni”alisema. 
 Katika baarifa yake kwa naibu waziri meneja wa Kiliwater, Prosper Kessy alisema uzalishaji wanakabiliwa na uzalishaji mdogo wa maji usiokidhi mahitaji kwani upo upungufu wa mita za ujazo 13,000 sawa na lita 13,000,000 kwa siku. 
 Alisema pia wanakabiliwa nupungufu wa mita za ujazo 22,000 sawa na litaza ujazo 22,000,000 wakati wa kiangazi na hivyo kuongeza tatizo la maji kwa wateja wake. 
 “Kiwango kikubwa cha asilimia 78 ya maji yasiyouzwa kutokana na uchakavu wa miundombinu,wazi wa maji,wateja wasio na mita na wale wenye mita lakini hutumia maji kiholela”alisema. 
 Hata hivyo alisema kampuni hiyo inahitaji zaidi y ash milioni 600 kwa ajili ya kuwafungia mita wateja wake kama njia moja wapo ya kuongeza mapato
 Naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge akikagua miradi ya maji katika wilaya ya Rombo.
 Mhandisi wa maji wilaya ya Rombo Andrew Tesha akitoa maelezo kwa naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge alipotembelea miradi ya maji katika wilaya hiyo.
 Naibu waziri wa maji Dk Mahenge akikagua mradi wa maji wa kilichopoeneo la hifadhi yam lima Kilimanjaro(KINAPA)
Naibu waziri Dk Mahenge akizungumza na mhandisi wa maji wilaya ya Rombo Andrew Tesha alipotembelea kisima cha maji katika kijiji cha Ushiri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 29, 2013

    hivi we waziri unawafikiria wananchi au unafikiria faida tuu swala la msingi wananchi wapate maji. Kwa hiyo bill inayolipwa 3,000 kwa mwezi sehemu ndogo ilobaki serikali ongeza sio we unataka kuongezewa mshahara tuu bila kufikiria wananchi hasa vijijni ambao wengi hawana kazi wanategemea hicho kishamba alichoachiwa na babu yake apate nusu ya debe kahawa, auze na haina bei ndio matumiz ya mwaka mzima. Jamani hebu kuweni na imani na wananchi so faida tuuuuu

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 30, 2013

    Waulize hao KILIWATER wanataka wananchi wachimbe mitaro ya maji kwa nguvu zao, watandike mabomba ya maji alafu wao waje wakusanye pesa kwa kuwawekea mita. Kwa nini msichimbe mitaro kwa gharama zenu na kufunga mabomba ya kisasa ili maji yasipotee bure. Mnategemea mabomba yaliyofungwa na mkoloni kupata faida?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...