Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akiwa na Mkuu mpya ya UNAMID Luteni Jenerali Paul Ignace Mella na kulia ni Luteni Jenerali Wynjones Mathew Kisamba Naibu Kamanda na ambaye pia alikuwa akikaimu nafasi ya Kamanda Mkuu UNAMID. Luteni Jenerali Mella na Luteni Jenerali Kisamba walikuwa hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa kwa ziara ya Kikazi na mafunzo. Lt. Jenerali Mella anasema yupo tayari kulitekeleza jukumu alilokabidhiwa na Umoja wa Mataifa na kwamba uteuzi wake katika wadhifa huo ni heshima kubwa wa Tanzania, Afrika, kwake yeye binfasi na zaidi kwa JWTZ ambayo mwaka itakuwa inatimizia miaka 50 tangu kuanzishwa kwake
Mkuu Mpya wa UNAMID Luteni Jenerali Mella akiwa katika picha ya pamoja na waambata wa kijeshi kutoka nchi za Afrika na kwingineko wakati alipotambulishwa kwao katika hafla fupi iliyoandawali na Uwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa. kutoka kushoto ni Naibu Mwakilishi Balozi Ramadhan Mwinyi, Lt. Jenerali Wynjones Kisamba, Balozi Tuvako Manongi, Lt. Jenerali Paul Mella na Maj. Jenerali Ngodi Mkuu wa jeshi la kulinda amani huko Lebano (UNFIL).
Mkuu mpya wa UNAMID, Luteni Jenerali Paul Mella akibadilishana mawazo na Kanali Mike Redmond ambaye ni Mwambata Jeshi wa Uingereza katika Umoja wa Mataifa.
Luteni Jenerali Mella akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Uwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa mataifa, wamo pia Balozi Tuvako Manoni, na Luteni Jenerali Kisamba.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 01, 2013

    Afande Mella you look more comfortable in military attire rather than suit. All the best.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 01, 2013

    Afande Mella you look more comfortable in military attire rather than suit. All the best.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...