Mmoja wa wapita njia akisoma moja ya bango lenye tangazo la tamasha la Filamu litakaloanza kufanyika jijini Mwanza leo katika uwanja wa Nyamagana.
================ ========= ========
JIJI la Mwanza kutwa nzima ya jana ilishuhudia hekaheka kubwa ya maandalizi ya
uzinduzi wa Tamasha la Wazi la Filamu Tanzania, maarufu kama ‘Grand Malt
Tanzania Open Film Festival’ ambalo litafanyika katika Uwanja wa Nyamagana, leo.
Wakazi wa Mwanza wanatarajia kuanza kushuhudia kitu kingine ambacho hakijawahi
kuonekana, wakati wa uzinduzi huo ambao unatarajiwa kufanyika mchana wa leo. Mratibu
wa Tamasha hilo aliye pia Mkurugenzi wa Sophia Records, Musa Kissoky, alisema wakazi
wa Mwanza na maeneo ya jirani wasubiri kuona vitu vya aina yake wakati wote wa
tamasha hilo linalotarajiwa kumalizika mwishoni mwa wiki.
Kissoky alisema, tamasha hilo ambalo litakuwa la bure kwa watu wote na kushirikisha
mastaa wa filamu hapa nchini, litakuwa la aina yake na kuwataka wakazi wa
Mwanza wajitokeze kwa wingi kushuhudia mambo yanayoendelea. Kila kitu kimekamilika, yaani tunaleta kitu tofauti ambacho watu watashangaa,
ndio maana mpaka sasa wengi wanapigwa na bumbuwazi kuhusu kile tutakachofanya
siku hiyo,” alisema.
Naye Meneja wa kinywaji cha Grand Malt walio wadhamini wakuu wa tamasha hilo,
Consolata Adam, alisema wameamua kufanya kweli zaidi kwani wanataka kuona
Watanzania wanapata kitu chenye uhakika. Tumejipanga katika hili na wala hatutanii. Tunawakaribisha watu wote wenye
mapenzi na filamu zetu za Tanzania kufika na kushuhudia tamasha hili ambalo
mwaka huu limeboreshwa zaidi,” alisema Consolata.
Naye Meneja Habari na Mawasiliano wa TBL, Edith Mushi, alisema, kutokana na
ubora wa kinywaji cha Grand Malt hata tamasha hilo litakuwa la aina yake na
litakaloiteka mikoa yote ya Kanda ya Ziwa. “Tumeona jinsi wananchi wanavyozipenda filamu za Tanzania, maarufu kama ‘Bongo
Movies’ na jinsi walivyo na kiu ya kuwaona wasanii wa filamu ana kwa ana, sasa
kazi kwao kuwashuhudia na kuona tamasha bora zaidi,” alisema.
Wasanii wakali wa Bongo Muvi wakiwemo Aunty Ezekiel, Vicent Kigosi ‘Ray’,
Jacqueline Wolper, Irene Uwoya, Jacob Steven ‘JB’, Mahsein Awadh ‘Dk Cheni’na
Issa Mussa ‘Cloud’ ni baadhi ya wasanii walioahidi kufanya kweli pia katika
tamasha hilo, huku bendi ya Extra Bongo chini ya Alli Choki ikitumbuiza.
Tamasha hilo la filamu limedhaminiwa na kinywaji cha Grand Malt kisicho na
kilevi ambacho kinazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...