 |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), akimkaribisha nchini Mhe. Sheikh Khalifa Al Hamad Al Sabah, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kuwait ambaye yupo nchini kwa ziara ya kikazi. |
 |
Mhe. Membe na Mhe. Al Sabah wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Ushirikiano katika masuala ya Siasa kati ya Tanzania na Kuwait. Tukio hilo lilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro Jijini Dar es Salaam tarehe 12 Julai, 2013. Kulia ni Bw. Benedict Msuya, Afisa Mambo ya Nje. |
 |
Mhe. Membe akizungumza na Mhe. Al Sabah (hayupo pichani) walipokutana. Wengine katika picha ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) (wa kwanza kushoto kwa Mhe. Membe), Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. Prof. Abillah Omar (kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (kushoto) |
 |
Mhe. Al Sabah akizungumza na Mhe. Membe (hayupo pichani). |
 |
Mhe. Al Sabah akifurahia zawadi aliyokabidhiwa na Mhe. Membe. |
 |
Picha ya pamoja. |
Mhe. Membe akimpatia maelekezo Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Naimi Aziz ambaye alishiriki mazungumzo kati ya Mhe. Membe na
Mhe. Al Sabah.
 |
Mhe. Prof. Omar (katikati) na Balozi Yahya (kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Maafisa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Kutoka kushoto ni Bw. Abas Mngwali, Bw. Hassan Mwamweta na Bi. Tagie Daisy Mwakawago. |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...