Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisaini nyongeza ya kwanza ya leseni ya utafutaji mafuta na gesi katika nchi kavu na kina cha bahari mashariki mwa Tanga) wanaoshuhudia ni wajumbe kutoka Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Watendaji wa TPDC, na watendaji kutoka kampuni ya AFREN.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akishikana mikono na Meneja wa kampuni ya AFREN kwa kanda ya Afrika Mashariki Bw.Jeremy Martin baada ya kusaini nyongeza ya kwanza ya leseni ili kuruhusu kampuni hiyo kuendelea kazi za utafutaji mafuta na gesi katika nchi kavu na kina cha bahari mashariki mwa Tanga. Kampuni ya AFREN imepata kibali cha kuendelea na shughuli za utafutaji mafuta na gesi katika eneo hilo kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limepewa nyongeza ya kwanza ya leseni (miaka minne) itakayoliwezesha Shirika hilo kuendelea na shughuli za utafutaji mafuta na gesi katika eneo la kina cha bahari na nchi kavu Mashariki mwa Tanga baada ya leseni ya awali kuisha muda wake.

Leseni hiyo imetolewa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo baada ya kuridhishwa na kazi za utafutaji mafuta na gesi zinazoendelea katika eneo hilo zinazofanywa na TPDC kwa kushirikiana na kampuni ya AFREN ya Uingereza.

Kutolewa kwa nyongeza ya kwanza ya leseni kutamwezesha mkandarasi kampuni ya AFREN mwenye ubia na TPDC kuendelea na shughuli za utafutaji mafuta na gesi katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuchimba kisima cha utafiti katika eneo la kina cha bahari mashariki mwa Tanga ifikapo katikati ya mwaka 2014.

Kampuni ya AFREN imepewa kazi ya ukandarasi wa utafutaji mafuta na gesi katika eneo hilo kutokana na kufanya kazi nzuri ya kukusanya data za kijiolojia na kijiofizikia ambazo ziliwezesha kutambua maumbile ya kijiolojia yenye viashiria vya kuwapo mkusanyiko wa mafuta au gesi katika eneo la Tanga.

Utolewaji wa leseni hiyo ulishuhudiwa na Bodi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), watendaji wa Wizara, watendaji wa TPDC, na watendaji wa kampuni ya AFREN.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...