Kamera ya Globu ya Jamii,mchana wa leo imeinasa taswira hii ya Mdau akiwa kaweka kishoka barabarani katika kijiji cha Mbwewe,Wilayani Handeni huku akiwa hana wasiwasi wowote kana kwamba kaweka kishoka hicho kwenye bombe moja la Shangingi huku magari kibao yakiendelea kupita kwenye barabara hiyo.Mdau unaionaje hii??

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 05, 2013

    hamna NOMA mdau kujipumzisha
    alisikia katika taarifa za habari OBAMA yupo bongo,usafiri wake utakuwa juu kwa juu na maelikopta, barabara zote zimefungwa kwa magari,kama bongo yetu nchi huru, kapata siku mbili za kujisikia yupo katika barabara za utelezi kama gomba la ndizi, siku za kawaida hapakaliki maeneo hayo.
    mikidadi mdau wa denmark

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 05, 2013

    Haina taizo, kwanza amekaa ukingoni kabisa mwa barabara, gari itafuata nini huko? Pili amekaa kushoto, hivyo magari yanayokuja anayaona ikiwa atatokea dereva mlevi.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 05, 2013

    hata mbuzi hawezi fanya hivyo. watanzania wamezidiwa akili na wanyama.
    gigo guy..

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 05, 2013

    SIO MTU HUYO, HIO HANDENI MNAIJUA NINYI? MWAFIKIRI MTU HUYO SIO KABISA, MARA NYINGI HILO DUDE HUONEKANA HAPO! CHEZEA TANGA WEWE!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 06, 2013

    Hali ya maisha inapokua ngumu watu hupoteza matumaini,mtu aliyepoteza matumaini uhai kwake hauna thamani tena,kuliona hili inataka weredi kidogo.Matukio mengi yenye kufanana na haya yanatokea na yatazidi kutokea huko nyumba kwa kasi hii tunayoenda nayo.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 06, 2013

    Ameghafilika in afilika.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 06, 2013

    Anyways...dogo amekaa kimachale, akiona namna gani..., "instinct" zitamrusha pembeni !

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 06, 2013

    kwa sisi wazoefu na wasafiri katika njia hizi napenda nitoe tahadhari kuwa wengine kama hawa wapo wakichagua gari za kuzisababishia ajali then wanaiiba. muwe macho sana. wapo hata usiku wa manane. wengine wanalala kama vile hawajitambui. ukilogwa ukasimama utaibiwa vitu.

    kama unaakili unajiuliza mtu mwenye afya njema kama hiyo anakaa barabarani kufanya nini?

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 06, 2013

    Kwani kuna ubaya gani kum-beep Israel????

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...