Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Angela Kairuki (katikati-mstari wa kwanza) akifuatana na Balozi wa Vietnam alimaliza muda wake wa kazi hapa nchini, Mhe. Nguyen Duy Thien (kulia), Mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini, Mhe. Balozi Juma Khalfan Mpango (kushoto mstari wa nyuma), Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Balozi Bertha Semu-Somi na Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Asia na Australasia, Bw. Omar Mjenga walipokuwa wanawasili katika Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro kwa ajili ya hafla fupi ya kumuaga Balozi Thien.
Mhe. Kairuki akizungumza kuhusu uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Vietnam wakati wa hafla  hiyo huku Balozi Thien na Mkewe wakimsikiliza.
Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Omar Mjenga akiwakaribisha wageni waalikwa kwenye hafla ya kumuaga Balozi Thien ambaye amemaliza muda wa kazi hapa nchini. Wengine katika picha ni Balozi Mpango na Balozi Semu-Somi.
Mhe. Balozi Nguyen Duy Thien na Mkewe wakimsikiliza Bw. Mjenga (hayupo pichani).
Mkuu wa Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini Balozi Mpango nae akizungumza machache wakati wa hafla hiyo huku Mhe. Kairuki, Balozi Thien na wageni wengine waalikwa wakimsikiliza.
Mhe. Kairuki akimkabidhi Balozi Thien na Mkewe zawadi ya picha ya kuchora ya Mji Mkongwe wa Zanzibar kama kumbukumbu yao kwa Tanzania.Picha na Reginald Philip.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Wachakachuziiis.

    ReplyDelete
  2. Hivi Waziri hakuongea ila mkurugenzi Msaidizi tu?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...