Bundi wa Ras Makunja hawana ukorofi na mtu, anadai Kamanda wa FFU Ughaibuni Ras Makunja. Baada ya kujichukulia tuzo ya kimataifa ya
bendi bora ya kiafrika barani ulaya,mkuu wa kikosi
kazi cha Ngoma Africa band aka FFU kamanda
Ras Makunja alikutwa akicheza na bundi wake
katika makao yake "Anunnaki Empire" na alipoulizwa
kulikoni awapende bundi hao na kwanini asifuge
ndege kama kasuku ? Kamanda Ras Makunja
alijibu eti "Bundi wake" hawana ukorofi na mtu
ni ndege wenye upendo tu tena watulivu kuliko
Kasuku. Kamanda Ras Makunja amedai kasuku
wana kelele sana..lakini Bundi wakimya na wapole.
Alipoendelea kuhojiwa akaamua kuuchuna.
Home
Unlabelled
bundi wangu hawana ukorofi na mtu, kasuku wana kelele - ras makunja
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Makunjas umejibu Vizuri sana!
ReplyDeleteNikiwa kama Mwana ndugu ktk familia yetu hii ya kuwakingia kifua Bundi ningependa uwaeleze Wajerumani sababu zingine hizi za ziada ni kwa nini ufuge Bundi badala ya ndege wengine?
Ni hivi waeleze haya Matano (5),
1.Ni njia ya kutoa mafunzo ya kujali viumbe na sio kwa maslahi kama kutarajia kuwachinja viumbe kwa vitoweo, Pana kila sababu ya kuwafundisha Binaadamu kuacha hulka mbaya saaana ya uchu kwa kufunga ndege au mifugo inayoliwa tu huku wakikwepa kufuga mifugo mingine mfano ndege kama hawa Bindi.
2.Bundi wamekuwa wakitengwa sana zaidi ya ndege wengine.
3.Ni somo kuifundisha Dunia jinsi ya kujali ''Minority societies za Viumbe kama hawa Bundi ambao ni wapweke sana Dunini'' kama walivyo hawa Bundi, na kuwa Dunia isiishie kwenye DEMOKRASIA za kupiga kura na Uchaguzi kwenye nchi zao peke yake.
4.Kuwahakikishia watu na hasa huku Afrika ya kuwa Bundi sio ndege wa Uchuro ama kuashiria Misiba, na kama ingekuwa ni kweli mawazo hayo nadhani Bwana Kamanda ktk Ukoo wako hadi sasa ungebaki peke yako tu.
5.Ni fundisho kumpa maisha ndege ama Kiumbe, tena aliyekuwa dis-advantaged (aliye dharauliwa na kutengwa na jamii) kama Bundi kuweza Kuishi nchini Ujerumani akila asali kwa maziwa Majuu!!!
LA MWISHO NI KUWA UWASILIANE NA MALAKA ZAUJEREMENI IKIWEZEKANA KANSELA ANGEL MARKELEL HIYO ''Anannuki Empire'' IPATE IWAKILISHI KULE BUNGENI UJEREMENI BUNDESTAG PIA MAMLAKA YA ANANNUKI EMPIRE IPEWE RUHUSA KUWA NA BENDERA YAKE!
Ras Makunjas Reason nyingine Mbili kubwa sana za kuwafuga Bundi:
ReplyDelete6.Rangi yake Nyeusi ni moja ya Rangi za Bendera ya Ujerumani.
7.Ktk Ngao ya Ujerumani (yaani kama ile Adam na Hawa yetu JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, ile Ngao ya UJERUMANI INA NDEGE AITWAYE TAI KIINGEREZA NI EAGLE AU VULTURE AMBAYE NI JAMII YA BUNDI!
Kamanda Ras Makunja,mbona kuna baadhi ya wadaku wanasema kuwa Bundi wako wamekuwa wakiwatisha majirani zako walizunguka "Anunnaki Empire"
ReplyDeleteBabaMtukutu Kamanda Mkuu wa FFU Field marshal Ras Makunja,chonde chonde kamanda mbona midudu hiyo macho yanatisha unaipendea
ReplyDeleteKamanda Ras Makunja inasemekana bundi wako wanakusaidia kufukuza msongomano wa wageni nyumbani kwako "Anunnaki Empire" a.k.a FFU Camp
ReplyDeleteYule ndege aliye katika nembo ya ujerumani ni aina ya FONEX
ReplyDeletebaba mtukutu kamanda mkuu wa ffu field marshal Ras Makunja mtawala wa viumbe wa ajabu Anunnaki Alien,wenzio wanafuga chiriku,kasuku,ninga tetele sasa wewe na bundi wako ! nyuma yake kuna siri gani? mkuu! midege hiyo sio ya kuishi nayo katika makazi ya binadamu kamanda
ReplyDeletemkuu wa kikosi kazi kamanda ras makunja kweli unatekeleza demokrasia ya ulaya kuwa kila kiumbe anastahili kuheshimiwa,wengine wanafuga mbwa wewe na bundi wako,tena unawatetea !
ReplyDeletePia nakubaliana nawe bundi ni ndege wakimya sana
Ras Makunja hao bundi wako kaa nao huko huko, ukija vekesheni bongo hawakubaliki. kwanza sijui utafikia wapi maana jumba lako la kariakoo pale Aggrey na Kongo umeshapiga bei, sasa kuna mzinga wa golofa. Yaani hata ungefikia hapo mwenyekiti wa mtaa angekushtaki kwa FFU wenzio pale Msimbazi. Unasema bundi mkimya, kivipi. anavyowanga usiku huwa huwasikii. au wa huko ughaibuni hawawangi usiku
ReplyDelete-Mwana Aggrey
wewe ! Mwana wa Agrey,
ReplyDeleteMadai yako ya kuwa hile nyumba ya kina kamanda imeuzwa si kweli kabisa,
Nyumba hiliyopo kariakoo Mchikichi/Kongo Namba 18 ya ghorofa 5
bado mali ya familia ya Kamanda wa FFU,Sema tu hii mududu Bundi anayo ifuga kwa kweli asije nayo kabisa Kariakoo,bundi wanatisha tena watatumalizia njiwa wetu.
Mdau
Jirani wa kamanda
Mchikichi street,Kariakoo
Nyumba yao akina Ras makunja iliopo
ReplyDeletemchikichi St.18 hawajauza lile ghorofa wanalimiliki familia yake.
Mdau
Mtoto wa jiji
Mtaa manyema
Anaefuga bundi ni mwanga mkubwa, lakini asiogopwe.
ReplyDeleteKamanda Ras Makunja ni mwanamuziki wa aina yake,
ReplyDelete