Mkuu
wa wilaya ya Makete Mhe. Josephine Matiro ambaye alikuwa mgeni rasmi katika
ufunguzi wa mradi huo ngazi ya wilaya akisikiliza maelezo ya mradi huo
kutoka SUMASESU
Mkurugenzi
wa shirika la SUMASESU Egnatio Mtawa akitoa maelezo kwa washiriki
kuhusu utambulisho wa mradi uitwao "Vijana wa makete na mapambano dhidi
ya maambukizi mapya ya virusi vya Ukimwi" katika ukumbi wa HIMA Makete
wakati wa utambulisho wa mradi huo ngazi ya wilaya Augusti 09, 2013.
Shirika la SUMASESU ndilo litakalotekeleza mradi huo kwa ushirikiano na
UNICEF
Washiriki wakisikiliza maelekezo kutoka kwa mkurugenzi wa SUMASESU (hayupo pichani)
Mratibu wa ukimwi halmashauri ya wilaya ya Makete CHAC Ester Lamosai(kushoto) akiwa na Anifa Mwakitalima kutoka SUMASESU
Mtaribu wa ukimwi sekta ya afya (DAC) Dk Shadrack Sanga akichangia hoja kwenye kikao hicho
Mkuu
wa wilaya ya Makete Mhe. Josephine Matiro akitoa hotuba yake wakati wa
ufunguzi wa mradi huo ngazi ya wilaya katika ukumbi wa HIMA Makete
Makamu mwenyekiti halmashauri ya wilaya ya Makete Jison Mbalizi akiahirisha kikao hicho
=======
Habari na picha na Edwin Moshi, Makete
Wadau wa mapambano dhidi ya virusi vya Ukimwi kwa vijana wilayani Makete mkoani Njombe wametakiwa kutoa elimu hiyo sanjari na elimu ya ujasiriamali kwa pamoja kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kupunguza ongezeko la maambukizi ya ugonjwa huo kwa kasi zaidi
Rai hiyo imetolewa na mkuu wa wilaya ya Makete Josephine Matiro wakati akifungua mradi wa vijana wa Makete na mapambano dhidi ya UKIMWI uliozinduliwa Ijumaa Agosti 9, 2013 ngazi ya wilaya, mradi ambao utatekelezwa na shirika la sumasesu kwa ufadhili wa UNICEF
Matiro amesema vijana wengi wamekuwa wakipatiwa elimu hiyo ya namna ya kujilinda na maambukizi mapya ya vvu na baada ya hapo wanakosa kazi ya kufanya hivyo kuwa rahisi kwao kujiingiza kwenye vitendo vitakavyowasababishia kupata vvu.
"Kijana anapewa elimu sawa lakini hana cha kufanya mwishowe akija mtu wa kuwarubuni hasa kifedha wanaingia kilaini kwa kuwa hana shughuli yeyote inayomuingizia kipato, mwishowe anaweza kupata vvu"alisema Matiro
Amewataka vijana kujiunga na vikundi mbalimbali ili waweze kupatiwa mikopo nafuu kwa ajili ya shughuli hasa kilimo kwa kuwa wakishajiunda na kutoa taarifa yeye kwa kushirikiana na halmashauri watawasaidia kupata mkopo ambapo wakati huo huo wakiwa na shughuli ya kufanya halafu wakapata elimu ya kujikinga na vvu itakuwa bora na yenye manufaa kwao.
Wadau walioshiriki katika kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa HIMA Makete akiwemo mratibu wa ukimwi sekta ya afya (DAC) Dk Shadrack Sanga amelitaka shirika hilo wakati wa kutekeleza mradi huo watoe elimu ya tohara kwa vijana wa kiume ambapo akiwataarifu wao kama idara ya afya wako tayari kuungana nao jambo lililoungwa mkono na kaimu mganga mkuu Boniphace Sanga ambaye alikuwepo kwenye kikao hicho.
Kwa upande wao shirika la SUMASESU kupitia kwa mkurugenzi Egnatio Mtawa alipongeza kwa ushirikiano uliooneshwa na wadau wote huku akimuahidi mkuu wa wilaya kuwa wataingiza mada ya ujasiriamali wakati wakitoa elimu ya ukimwi kwa vijana ili iwasaidie huku akiahidi kushirikiana na kila wahusika ili mradi huo ufanikiwe
Mradi huo utakaotekelezwa hadi Julai 2015, utahusisha kata za Ipelele, Iniho, Iwawa, Isapulano na Kitulo
ReplyDeleteWAKUU MTANIWIA RADHI HAYO MA-POSE YA DC MATIKO NA MRATIBU WA UKIMWI LAMOSAI MIMI NI HOI.
SIJUI NIKIULIZA KAMA WAMEOLEWA AU LAA NITAKUWA NIMECHAFUA HALI YA HEWA UKUMBINI AU VIPI.
NATANGULIZA SAMAHANI WAKUU NIMESHINDWA KUJIZUIA