KAMPUNI ya bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Kilimanjaro Premium Lager, inang'oa nanga kwa awamu ya pili ya Tamasha la Muziki ‘Kili Music Tour 2013’ ambapo wikiendi hii litarindima ndani ya mjini Mwanza.

Wasanii hao ni pamoja na Diamond, Snura Mushi, Professor J, Lady Jay Dee, Roma, Dabo, Bob Junior,Ben Pol, Kala Jeremiah, Fid Q na AT.
Matamasha ya Kili Music Tour 2013 yalikuwa yamepumzika kwa muda wa mwezi mmoja na sasa yanarejea tena kwa kishindo kwenye mikoa mitano iliyobaki.
“Tunashukuru kuwa watanzania wamelipokea vizuri tamasha hili kwa moyo mkunjufu kabisa na walishiriki kikamilifu kwenye mikoa ya Dodoma, Tanga na Kilimanjaro, tuliamua kupumzika kwa muda wa mwezi mmoja kwa ajili ya kupisha mfungo, na hii ilitupa muda mzuri wa kujipanga na kuboresha zaidi matamasha haya hivyo basi tunategemea Mwanza itajumuika nasi ipasavyo kufanikisha tamasha litakalofanyika mkoani hapo siku ya Jumamosi ya tarehe 17 mwezi huu.” Alisema George Kavishe ambaye ni Meneja wa bia ya Kilimanjaro.

Kwa niaba ya wasanii wenzake msanii mahiri wa bongo fleva Professor Jay “Joseph Haule” amewataka wakazi wa Mwanza kujitokeza kwa wingi huku akisema “tumejiandaa vizuri sana kutoa burudani kali kabisa, lazima mji wa Mwanza utikisike kwa kishindo cha bonge la kiburudisho kwa style tuipendayo ya “kikwetukwetu”.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...