Geti kuu la hoteli ya kitalii ya Ledger Plaza-Bahari Beach jijini Dar es salaam ambayo imefunguliwa hivi karibuni na kuwa kivutio kwa wadau wa kila aina hasa siku za Jumapili na Sikukuu. Tofauti na hoteli kibao za ufukweni hapa kiingilio ni bure ila unatozwa huduma kama vile kutumia bwawa la kuogelea, chakula na michezo ya watoto
 Ankal akiwa na wadau Bahari Beach katika Iddi tatu leo Jumapili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Ankal,
    Duh! Kweli wadau wa Bongo starehe ni tambarare, sie huku ughaibuni stress kibao kwa kubeba boxi bila mapumziko ya uhakika kama hayo ya bembezoni ya bahari.

    Lazima nikitua Bongo niende moja kwa moja Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar-es-Salaam kwa mapumziko ya uhakika mabli kabisa na 'mihangaiko ya stress ya Ughaibuni.

    Mdau
    Ughaibuni.

    ReplyDelete
  2. Kaka michuzi huyo ni Daudi Lembuya aka Mr. Dee sio Dj venture

    ReplyDelete
  3. Ankal acha Ubahili!

    Sasa Mjomba masifuri yote unayo tengeneza kwenye kazi zako kutokea kule Ofisi yako Serikalini hadi kwenye Libeneke halafu wewe na Familia ktk Idd unawapeleka Hoteli ya kiingilio cha Bure?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...