Picha na Habari na Faustine Ruta, Bukoba
Timu ya BILELE FC  imelazimika kupigana kufa na kupona ili waweze kutinga hatua ya fainali katika michuano ya Kombe la Kagasheki ikicheza dakika 90 na timu ya Kitendaguro fc bila ya kufungana. Baada ya kuongezwa 30 Bilele FC imeweza kuifunga timu hiyo maarufu kwa jina la Makhirikhiri yeye maskani yake Kitendaguro - Kibeta. 
Bao la pekee la timu ya Bilele limefungwa dakika kipindi cha kwanza cha dakika 120 na mchezaji Ndomondo, huku wakicheza pungufu baada ya mwenzao kupewa kadi nyekundu katika kipindi cha pili cha dakika 90. 
Ushindi huu unawasogeza Bilele hatua ya Fainali wakimsubiri mshindi wa kesho kati ya timu ya Kashai Fc na timu Rwamishenye Fc mtanange utakaochezwa kesho Jumatano saa 10.00 jioni hapo hapo uwanja wa Kaitaba.

Timu zikisalimiana muda mfupi kabla ya mtanange kuanza

Timu zikisalimiana muda mfupi kabla ya mtanange kuanza hapa kwenye Uwanja wa Kaitaba
Picha ya pamoja Waamuzi wa mtanange huu na manahodha wa timu 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Huu ndio uwanja unaotumika kwa premier league? Kama ndio huu malalamiko ya timu kuhusu kaitaba ni ya kufanyia kazi haraka. Unawezaje kuweka mpira chini ktk hali kama hiyo!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...