Ndege Ndogo ya Shirika binafsi la Ndege la TANZANAIR iliyokuwa ikitokea Mjini Bukoba kuelekea Jijini Dar es Salaam kupitia Zanzibar, imelazimika kutua katikati ya Ziwa Manyara lililopo Mkoani Arusha ili kunusuru abiria wake sita (6) waliokuwamo katika ndege hiyo baada ya kupatwa na hitilafu kwa kuzima ghafla kwa Injini moja wakati ikiwa hewani. 
Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Kamanda Liberatus Sabas amethibitisha kutokea kwa ajali hilo majira ya saa 2.35 asubuhi maeneo ya Lambi, kusini mwa wilaya ya Babati. 
 Kamanda Sabas  amesema rubani wa ndege aliyetajwa kwa jina moja la Kondo, ambaye hakudhurika katika ajali hiyo, alitaka kutua ghafla katika viwanja vya  Arusha na Manyara baada ya kutokea hitilafu hiyo, lakini alishindwa baada ya kuona mtikisiko ukizidi na kuamua kuielekeza ndege hiyo katikati ya Ziwa hilo, ambapo alifanikiwa kutua salama.
Baadhi ya Boti na mitumbwi iliyokuwa karibu ilisogea na kutoa msaada wa kubeba abiria hao na kuwasogeza nchi kavu na baadaye ilifika Helikopta ambayo iliweza kutoa msaada zaidi.

DJ SEKNdege ya shirika la ndege la Tanzanianair ikiwa imetua katika maji ziwa Manyara jana na abiria saba kukimbizwa hospitali mkoani Arusha baada ya injini moja kushindwa kufanya kazi ikiwa angani.DJ SEK BLOG


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Rubani tukupe hongera kwa jitahada kuokoa maisha ya wananchi na wahuisika wa vyombo kama hivyo kuweni makini kwa kufanya service ya uhakika kuepuka ajali zinazoweza kuepukika hongera rubani kondo

    ReplyDelete
  2. Kondo namfahamu ni rubani mzuri sana. Niliwahi kusafiri kwa ndege yake mwaka 1989 tukiwa na mzee Aboud Jumbe mkewe na bodyguard wake akiitwa Abubakar Mbange. Kama ni Kondo huyu huyu basi ni rubani wa kutegemewa mzee huyu.
    Poleni kwa yaliyowapata abiria na hongera mzee Kondo kwa kuponya maisha na kuonyesha ukongwe wako angani

    ReplyDelete
  3. Hongera sana Rubani.

    ReplyDelete
  4. Kondo umeonyesha umahiri na ujasiri uliotukuka ktk kuhimili tatizo lililojitokeza na kuweza kuokoa maisha ya abiria wako! Unastahili pongezi na sifa big up captain Kondo

    ReplyDelete
  5. Capt Kondo unastahili pongezi

    ReplyDelete
  6. Matendo yake Mungu ni ya ajabu sana. Tumpe sifa daima kwa kunusuru maisha ya ndugu zetu hawa. Hongera pia kwa Bw. Kondo kwa jitihada za pekee za kuokoa maisha ya hao abiria

    ReplyDelete
  7. Mungu ameonekana pia, ni jambo la kushukuru, poleni kwa ajali ila pia hongeren mmepona. God is great. proscovia

    ReplyDelete
  8. God is goodoo

    ReplyDelete
  9. Yeah,God is good all the time..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...