Na Mwandishi Wetu
UONGOZI wa Boom FC umelishukuru Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kwa kuipatia msaada wa Sh 5,125,000 kwa ajili ya uendeshaji wa timu hiyo katika Ligi Daraja la Pili Mkoa wa Dar es Salaam.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Katibu mkuu wa Boom FC, Duni Mibavu amesema fedha hizo zitasaidia timu kufanya vizuri katika ligi na kuwapa morali wachezaji ili kuhakikisha timu hiyo inacheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao.
“Tunawashukuru wenzetu wa NSSF chini ya Mkurugenzi wake Dk. Ramadhan Dau kwa msaada mkubwa walioutupatia, hii inaonyesha ni jinsi gani walivyoguswa na na kilio chetu na kuamua kutusaidia ili tufanye vizuri,” alisema.
Duni ameomba na mashirika mengine pamoja na makampuni mbalimbali nayo kuiga mfano wa NSSF katika kuzisaidia timu za madaraja ya chini ili nazo zifanye vizuri.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...