Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Isaac J. Nantanga akizungumza na Waandishi wa Habari  jijini Dar es Salaam kuhusu mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania kuwarejesha kwao wakimbizi waliokuwa hapa nchini.  Kulia ni  Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Uratibu wa Mawasiliano ya Serikali, Bi. Zamaradi Kawawa.
-----------------------------------
Serikali ya Tanzania imewarejesha kwao kwa hiari wakimbizi wapatao 569,018 toka nchi za Maziwa Makuu waliokuwa wamehifadhiwa hapa nchini kutokana na machafuko katika nchi zao.  Kati ya hao 502,358 walitoka nchini Burundi na 66,660, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.  Wakimbizi hawa wamerejeshwa kwao kufuatia zoezi lililoanzishwa rasmi mwaka 2002 kwa wakimbizi toka Burundi na mwaka 2005 kwa wakimbizi toka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRS), baada ya usalama katika nchi zao kuimarika.
Sambamba na mafanikio haya, pia kambi 12 kati ya 13 zilizokuwa zikitumika kuwahifadhi wakimbizi hawa zimefungwa, na hadi sasa ni kambi moja tu ya wakimbizi ya Nyurugusu, wilayani Kasulu mkoani Kigoma ndiyo iliyobakia ikiwahifadhi wakimbizi kutoka DRC (63,728), Burundi (4,153) na nchi nyingine mchanganyiko za Kiafrika (212).
Tanzania inajulikana kimataifa kama nchi mojawapo ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kutoa hifadhi kwa wakimbizi wanaokimbia nchi zao kutokana na machafuko ya kiaiasa ambapo mwaka 1995 idadi yao ilifikia zaidi ya milioni moja.
Lengo la Serikali ni kuona kuwa suala la kuhifadhi wakimbizi hapa nchini linafikia ukomo na juhudi zinaendelea kuona kuwa hata Kambi ya Nyarugusu ambayo ndiyo kambi pekee iliyobakia inafungwa baada ya wakimbizi walio katika kambi hiyo kurejeshwa kwao, pale hali ya usalama nchini DRC itakapokuwa imeimarika.Kuondoka kwa wakimbizi hawa sasa kunatoa nafasi kwa Serikali na wananchi kutumia kwa shughuli nyingine za kimaendeleo maeneo makubwa yaliyokuwa yanatumika kuhifadhi wakimbizi, lakini pia kunatoa nafasi nzuri ya kuweza kukabiliana na changamoto za kiusalama katika maeneo hayo ambayo yapo katika mikoa ya mpakani mwa nchi.Serikali inapenda kuishukuru Jumuiya ya Kimataifa kupitia Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), kwa misaada ya hali na mali waliyotoa na wanayoendelea kutoa kusaidia hifadhi ya wakimbizi hapa nchini. Pia Watanzani wote na hasa wale wa mikoa ya Katavi, Kigoma na Kagera kwa ushirikiano waliotoa kwa wakimbizi waliokuwa wamehifadhiwa katika maeneo yao, na nchi za Burundi, Congo kwa ushirikiano wao uliowezesha kuwarejesha raia wao waliokuwa wamehifadhiwa hapa nchini.
Mashirika mengine ambayo pia yalihusika na yanaendelea kutoa huduma za kibinadamu kwa wakimbizi ni pamoja na Shirika la Chakula Duniani (WFP), Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Watoto (UNICEF), Kamati ya Kimataifa ya Uokozi (IRC), na Shirila la Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS).
Imeandaliwa na Felix Mwagara
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. nyinyi wabaguzi tu hamna lolote !!wapeni uraia waafrika wenzenu, kama nyinyi mnavyolilia uraia nchi za ulaya na sio kuwarudisha makwao

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ndo tushawarudisha, we unasemaje sasa? Ushaambiwa kwa hiari hawakushikiwa mtutu wa bunduki, bora kwa maana tunawahifadhi miaka na miaka mwisho wa cku wanatugeuka.

      Delete
  2. Wewe sasa nikosa mtu kumrudisha kwao na kama ni ubaguzi acha ufanyike,kwani IZRAEL SI NAO WANAWARUDISHA WAETHIOPIA NA SIO TIO NA NCHI ZINGINE,WEWE WATU WOTE HAO UNAWEZA KUWAPA URAIA,,WOTE? NCHI GANI DUNIANI IMEFANYA HIVYO AU NA WEWE NIMYARWANDA UNALETA CHUKI ZA BINAFSI.SEMA NI NCHI GANI IMETOA URAIA KWA IDADI KAMA HIYO ,RAIS WETU JUZI KASEMA KASHATOA URAIA KWA WAKIMBIZI WENGI TU SASA WEWE UNATAKA NINI?-UPOLE WETU NDIO UNAFANYA NYIE WENGINE MNAKOSA SHUKRANI KWA MUDA AMBAO WALISHAKAA NCHI ULITAKIWA KUSHUKURU KUWA WAMERUDI SALAMA NA WALIKUWA HAWABUGUDHIWI.SASA IMEKUWA SHUKRANI YA PUNDA.SISI TUMEFIKIA HAPO KAMA UNAWEZA WAPELEKE NCHINI KWENU

    ReplyDelete
  3. Acha warudi kwao,majitu yenyewe yanasaidiwa then yanarudi kumtukana rais wetu JK,hao hao wakimbizi wameongeza ujambazi mikoa ya Kagera na Kigoma.Hata waliobaki nao warudishwe kwao tu maana hawana shukrani hata kidogo kushinda punje ya haladari

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...