Mwenyekiti wa Halmashauri ya  Iringa na diwani wa kata ya Nzihi Bw Stivin Mhapa kushoto akimpongeza Bw Jackson Kiswaga kwa  kujitolea  kusaidia elimu  shule  aliyosoma ya Nyamihuu jimbo la Kalenga 

Baadhi ya wahitimu  wa darasa la saba katika  mahafali ya  34  shule ya Msingi Nyamihuu  wakisikiliza ahadi ya Bw Kiswaga ya  kusomesha  watoto  watatu  elimu ya sekondari 
mkazi  wa Kijiji cha Nyamihuu anayeishi  jijini Dar es Salaam  Bw  Jackson Kiswaga ambae ni mkuu  wa kitengo  cha M- Pesa ukuzaji  wa biashara akimkabidhi  cheti  cha uongozi  bora  na uchapakazi mwanafunzi mhitimu  wa darasa la  saba Revina Mwendele leo
Mwanafunzi Ajuaye Ngeve  mhitimu wa darasa la  saba  shule ya Msingi Nyamihuu akikabidhiwa  cheti  chake na mgeni wa  heshima katika mahafali ya 34 ya shule  hiyo Bw Jackson Kiswaga  leo

Na Francis Godwin
MWENYEKITI wa  Halmashauri ya  wilaya ya  Iringa na diwani wa kata ya Nzihi  jimbo la Kalenga  Bw  Stivin Mhapa  amempongeza  mkazi wa kijiji  cha Nyamihuu anayeishi  jijini Dar es Salaam  Bw  Jackson Kiswaga  kwa  ahadi yake ya  kujitolea  kusomesha  sekondari  wanafunzi  watatu  wa  shule  hiyo ambao  watafanya  vizuri  katika matokeo ya mtihani wa Taifa  wa Darasa la  saba  mwaka 2013 na  kushindwa ada ya kwenda  Sekondari.
Mhapa  ametoa  pongezi hizo  leo  katika mahafali ya  34  ya  shule  ya Msingi Nyamihuu mara  baada ya Bw  Kiswaga  kutoa  hutuba yake  na kuahidi kusomesha  wanafunzi hao .
Alisema  kuwa kilichofanya na Kiswaga ni mfano  wa  kuigwa na  wengine na kuwataka  wazazi  kuhakikisha  wanawasimamia  vema  watoto  wao  ili kuendelea na masomo  zaidi.
Pia  Mhapa  alitaka  msaada  huo  kusimamiwa  vizuri na  viongozi wa  kijiji na kuwa  wale  watakaochaguliwa  kunufaika na msaada  huo ni vema majina yao yakatangazwa katika mkutano  wa hadhara  ili kila mwananchi aweze kujua na kama kuna uchakachuaji  basi kufahamika.
Kwani  alisema baadhi ya  watu  wamekuwa  si waaminifu na  kuwaacha  walengwa na kuwapa nafasi  wenye  uwezo badala ya  wale  wasio na uwezo.
Kwa  upande wake  Kiswaga  alisema mbali ya ahadi  hiyo pia ataichangia  shule  hiyo kiasi cha Tsh 500,000 kwa ajili ya kuchangia ununuzi wa madawati  katika  shule  hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...