LEO UMETIMIZA MWAKA MMOJA KAMILI TOKA ULIPOTUACHA GHAFLA BAADA YA KUUGUA GHAFLA SANA. HATUNA CHA KUSEMA TUNAAMINI UMEKWENDA KUTUANDALIA MAKAO YA MILELE ILI SISI NASI TUKUTANE HUKO, MAANA HUKU DUNIANI TUKO MATEMBEZINI TU.
VICK UMETUACHA KATIKA MAJONZI MAKUBWA NA MASWALI MENGI! KIFO CHAKO KIMETUSHTUA WENGI MAANA KIMETOKEA MIEZI MIWILI TU BAADA YA HARUSI YAKO. LAKINI KWAKUWA TU WAKRISTU TUNAAMINI MUNGU AMECHUMA UA ZURI KATIKA BUSTANI YAKE NA KAZI YAKE SIKU ZOTE HAINA MAKOSA. TUMEKUBALI YOTE! TUPO KAMA ULIVYOTUACHA, TUNAENDELEA KUKUENZI KWA HAYO INGAWAJE BADO MAJARIBU NI MENGI.
UNAKUMBUKWA NA MIMI MAMA YAKO LYDIA, BABA JAPHET MBWANA, MUMEO MPENZI EMMANUEL KILATO, NDUGUZO MERCY, GODFREY NA VIOLLA, MAMA MKUBWA, WAJOMBA, WAKWE ZAKO, WANA UKOO WOTE, MAJIRANI WA LUMALA - MWANZA, GEITA NA DODOMA, WAFANYAKAZI BENKI KUU MWANZA, WANAJUMUIA YA FIDEL – PAROKIA YA PASIANSI, NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI.
 MISA YA KUMALIZA MSIBA ITAKUWA NYUMBANI KWAO LUMALA B TAREHE 7/9/2013 SIKU YA JUMAMOSI SAA NANE MCHANA, KARIBUNI SANA
RAHA YA MILELE UMPE EEH! BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWNGAZIE, APUMZIKE KWA AMANI
AMINA!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Liydia poleni sana Mungu aendelee kuwatieni nguvu na aendelee kuwafariji maana yeye ndie mfariji wa kweli

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...