Washiriki wa maonesho, wananchi mbalimbali wakiingia ndani ya Uwanja wa CCM Kirumba kwa maandamano ya kufunga maadhimisho Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani . Maadhimisho ya Nenda kwa Usalama yamefungwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Gerson Lwenge baada ya kufunguliwa mwanzoni mwa wiki hii na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “USALAMA BARABARANI UNAANZA NA MIMI, WEWE NA SISI SOTE”. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira kutoka Makao Makuu ya Wakala wa Barabarani Tanzania (Tanroads), Zafarani Madayi akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Gerson Lwenge (wapili kushoto) jinsi Tanroads inavyoweza kutengeneza barabara bora na zenye alama za usalama kwa lengo la kuondoa ajali mbalimbali zinazoweza kutoa barabarani kabla ya kuyafunga maonesho hayo yaliyokuwa yanafanyika katika Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza. Watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani, Pereira Ame Silima. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “USALAMA BARABARANI UNAANZA NA MIMI, WEWE NA SISI SOTE”. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, DCP Mohamed Mpinga, akikionesha kitabu cha taaluma ya ufundishaji wa madereva kilichozinduliwa na mgeni rasmi Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Gerson Lwenge, kabla ya kufunga maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama yaliyokuwa yanafanyika jijini Mwanza. Kulia (waliokaa) ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani, Pereira Ame Silima. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “USALAMA BARABARANI UNAANZA NA MIMI, WEWE NA SISI SOTE”. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Mkurugenzi wa Radio One, Deogratius Rweyunga (kushoto) akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani, Pereira Ame Silima, baada ya kupokea cheti cha kuthamini mchango wa Radio hiyo iliyopo Dar es Salaam kwa kutangaza habari mbalimbali za usalama barabarani.  Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani yamefungwa rasmi na Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Gerson Lwenge, jijini Mwanza leo. Kauli mbiu ya Maadhimisho ya mwaka huu ni “USALAMA BARABARANI UNAANZA NA MIMI, WEWE NA SISI SOTE”. 
Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...