Baadhi ya wachezaji wa timu ya Kamba ya Ofisi ya Makamu wa Rais, wakishangilia ushindi wao baada ya kuwaburuza timu ya Katiba na Sheria katika raundi mbili mfululizo, katika mchezo wao uliochezwa leo asubuhi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha UDOM mjini Dodoma.
Wachezaji wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Kamba wakionyesha uwezo wao wa kutunisha misuri kuwaburuza wapinzani wao wa timu ya Katiba na Sheria, wakati wa mchezo wao uliochezwa leo asubuhi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha UDOM mjini Dodoma. Katika mchezo huo Ofisi ya Makamu wa Rais ilishinda kwa raundi mbili mfululizo.
Wachezaji wa timu ya Katiba na Sheria, Kamba wakijaribu kugangamala kuwazuia wapinzani wao wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais, wakati wa mchezo wao uliochezwa leo asubuhi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha UDOM mjini Dodoma. Katika mchezo huo Ofisi ya Makamu wa Rais ilishinda kwa raundi mbili mfululizo.
Wachezaji wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais (kulia), Kamba wakionyeshana umwamba wapinzani wao wa timu ya Katiba na Sheria, wakati wa mchezo wao uliochezwa leo asubuhi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha UDOM mjini Dodoma. Katika mchezo huo Ofisi ya Makamu wa Rais ilishinda kwa raundi mbili mfululizo.
Wachezaji wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais Kamba wanawake, wakishangilia ushindi wa chee waliopata baada ya wapinzani wao Katiba na Sheria kuingia mitini.
Wachezaji wa timu ya Ofisi ya Makamu wa Rais, Kamba na Soka, wakiwa katika picha ya pamoja, baada ya timu zao za Kamba (KE) na (ME) kushinda katika michezo yao.
Kamba wananwake Bunge na Uchukuzi, wakiburuzana. Katika mechi hii, Bunge walishinda baada ya kuwaburuza wenzao mara mbili mfululizo.
'RAHA YA USHINDI BAO', Wachezaji wa timu ya Kamba ya Habari, wanaume wakishangilia ushindi wao baada ya kuwaburuza mara mbili mfululizo wapinzani wao, Uhamiaji katika mchezo wao uliochezwa leo asubuhi, kwenye viwanja vya Chuo Kikuu UDOM, mjini Dodoma.
Wachezaji wa timu ya Habari (kushoto), Kamba wakionyeshana umwamba wapinzani wao wa timu ya Uhamiaji, wakati wa mchezo wao uliochezwa leo asubuhi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha UDOM mjini Dodoma. Katika mchezo huo Habari ilishinda kwa raundi mbili mfululizo.
Mchezaji wa timu ya wanawake Kamba ya Uhamiaji, akibebwa kuwekwa pembeni ili kupatiwa huduma ya kwanza baada ya kuanguka wakati walipoburuzwa na wenzao wa Habari na kuwavuta mara mbili mfululizo, katika mchezo wao uliochezwa kwenye Viwanja vya Chuo Kikuu cha UDOM leo asubuhi.
Uhamiaji wanawake wakijaribu kugangamala kuwazuia Habari, lakini waliburuzwa katia mechi hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...