Wakati upepo mzuri wa kipindi cha joto kutoka bahari ya Hindi ukipuliza, uzinduzi wa mgahawa mjini Zanzibar, Six Degrees South, ulikuwa hauna mfano! Huku kukiwa na fataki za ndani, chupa za Moet zikifunguliwa kwa madaha usiku kucha mpaka mida ya usubuhi, uzinduzi wa Six Degrees South uliwaacha wengi mjini Zanzibar wamepigwa na butwa wakiwa hawana la kusema.
Six Degrees South ipo eneo la mji mkongwe na inawapa wageni utulivu wa hali ya juu ili kuwawezesha kupumzika na kujichanganya. Ukichanganya mazingira ya utulivu na na huduma ya bure ya mtandao wa internet, sehemu hii inamfaa mtu yoyote kupata kinywaji anachopendelea na vitafunwa. Mgahawa una vibaraza kwenye ghorofa tatu vyenye eneo kubwa kwa ajili ya wageni kutazama jua likizima kwenye mandhari ya Bahari ya Hindi. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA





Mji mkongwe ni mkubwa, sema hasa ni sehemu gani ya mji mkongwe ulipo mgahawa huu!!!!!!!!
ReplyDeleteHizo picha za mwisho inaonekana ni pale zanzibar house,karibu na wizara ya utumishi
ReplyDelete