Ningependa kuwauliza wale watanzania walio Marekani kama tunaweza ku-share ni kadi gani za simu zenye dakika nyingi kupiga Bongo cell phones.   Wengi wetu kupiga simu nyumbani ni muhimu, sio kila siku ila mara kwa mara. Na gharama za kadi kiasi fulani ni kubwa, mimi kadi ambazo natumia online nyingi ni 17c per minute (.17/min).. which means unapata karibia dakika 58 kwa $10.. Naelewa kuna apps kama viber ambazo zinasaidia kiasi fulani, ila ni vigumu kumwambia bibi akiwa Masasi kwamba weka viber kwenye simu. 
Kwa hiyo kama mtu anajua website gani wana kadi zenye deal zenye rates nzuri kupiga Tanzania please naomba tuambizane. Kama itakuwa ya mtanzania itakuwa bora zaidi, kuinuana muhimu. Au kama kuna means za kupiga simu besides kadi mtu unajua please let us share.
Napatikana jmakwanga@yahoo.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 21 mpaka sasa

  1. Natumiaga hii:
    www.ezcalls.com
    Rates zake ni different kutokana na mtandao utakaopiga kwa mfano kwa Tigo unaweza kuongea dakika 111 kwa dola 10.
    Natumaini hii itakusaidia.
    Kutoka kwa,
    dailylifeandliving.blogspot.com

    ReplyDelete
  2. mdau makwanga ukweli wa mambo ulimwengu mzima VOCHA-TIGO ndo rahisi kinachotakiwa wajipange next-level kujinoa na mtandao wa kadi za kitaifa ndani na kimataifa kwa soko la nje haswa kwenu usa wadau wa bongo wapo wengi.
    mikidadi-denmark

    ReplyDelete
  3. Mimi natumia vip communications

    ReplyDelete
  4. Tumia Umojaphone

    ReplyDelete
  5. jaribu www.rebtel.com also ina rate nzuri na ni rahisi kuongezea hela.

    ReplyDelete
  6. boss revolution $5-voda 55min,tigo 34min,airtel 20min

    ReplyDelete
  7. Bass revolution" igoogle hiyo iko poa

    ReplyDelete
  8. kadi? we no longer use that where I am. That was about 10 years ago.

    What is it actually?

    ReplyDelete
  9. UNAPIGA SIMU BONGO UNATAFUTA NINI?KURUDIA VUMBI?PIGA UK.

    ReplyDelete
  10. Tabu Tanzania inachaji pesa nyingi kampuni hizi zilizo bei poa, inashangaza rates za kupiga TZ hata Europe wenzetu wakenya na waganda kwa dakika moja kwetu kuongea either mobile au landline. Wao ni mara tatu au nne madakika kwa bei hiyo hiyo.

    Tanzania inabidi ipunguze kuwachaji pesa nyingi hizi kampuni ili watupunguzie bei za kupiga per minute.

    ReplyDelete
  11. Mdau,hotvoip unaweza kupiga kwenda mitandao yote ya simu za mkononi Tanzania kwa gharama ya dola za kimarekani 0.068 kwa dakika,unachotakiwa ni kudownload hiyo software kisha kujisajili na kisha unanunua credits na baada ya hapo unaweza kupiga simu.

    ReplyDelete
  12. kama unatumia Boost mobile, basi lipa zaidi kidogo ya bill yako na utapiga bila kutafuta CARD ZA SIMU ni kuinua tu na kubonyeza namba na inadumu muda mrefu karibu siku 15 hata kama unapiga kilasiku dakika mbili au jiunge na Westen union, kwa kutuma hela tu huko Tanzania, pia wanakuwekea AIRTIME kwenye card yao ambayo utatumia kama vocha na inadumu muda mrefu na conection yake ni beautiful.

    ReplyDelete
  13. Sasa, bongo si wana mtandao? na simu karibu zote zina mtandao Bongo. Kwa nini utumie makadi tena wakati kama wote wawili mna download SKYPE, WHATSAPP, Yahoo messenger, LINE, VIBER, WECHAT, mnaweza kuongea BURE na kama simu zao ni smartphone, hata unaweza kuongea huku unawaona. Hizi mikadi yamepitwa na wakati.

    ReplyDelete
  14. umeshaambiwa bibi hawezi kuweka hozo viber stuff!

    ReplyDelete
  15. kwa haraka nmepitia options zilizotolewa na inaonekana amantel.com wapo juu!

    ReplyDelete
  16. Nunua MAgic JAck na huku mnunulie mtu MAgic JAck utaongea weee mbaka baaasi

    ReplyDelete
  17. Acha ubahili wanunulie ndugu/jamaa zako smart phones. Initial cost itakuwa kubwa lakini wakisha kuwa na smart phones, internet kwa simu Tanzania ni bei sawa na bure. Kwa hiyo wakishakuwa na smartphones, utasahau kununua kadi, na maisha yataenda vizuri. Mimi nilifanya hivyo, ndugu/marafiki zangu ambao natakiwa kuongea nao mara kwa mara niliwapatia zawadi za smart phones. Kwa kufanya hivyo niliokoa pesa nyingi ambayo ningetumia kununua kadi. Maana najua hauwezi kuwa na ndugu wa kuwasiliana nao zaidi ya kumi. Utakuwa na ndugu wengi lakini si lazima uwasiliane na wote.

    Kwa kutumia kadi unaweza kutumia USD 10 kwa siku. Kwa mwezi ni USD 300. Kwa hapa ninakoishi (Sweden) kiasi hicho cha pesa kinatosha kununua simu 3 ambazo unaweza kudownload viber, skype, n.k.

    Ákili ni nywele..........

    ReplyDelete

  18. Akili ni nywele...., kila mtu ana kipara.

    ReplyDelete
  19. Makwanga acha kuichungulia Sarafu ya DOLA kama hivyo!

    Unautia aibu Ugenini, ni kuwa gharama za maisha ni dunia nzima huwezi kuishi CHINI YA DOLA MOJA KWA SIKU KAMA UPO AFRIKA kumbuka upo Marekani kwa Obama!!!

    ReplyDelete
  20. Ndugu Makwanga hivi wewe utakuwa unatokea mkoa wa Kilimanjaro?

    Una onekana Mchumi sana!

    ReplyDelete
  21. Makwanga upo Marekani kwa muda mrefu sana!

    Kama unataka msaada wa mawazo kwa nini usipige Simu namba 911 upate majibu?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...