Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa Juma Ali Simai akiweka jiwe la msingi ujenzi wa ofisi ya kata ya Tandala.
 afisa mtendaji kata ya Tandala Ambele Sanga akisoma taarifa ya ujenzi huo
Na Edwin Moshi, Makete 
Ujenzi wa ofisi ya kata ya Tandala wilayani Makete mkoani Njombe umewekwa jiwe la msingi na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Juma Ali Simai huku akisisitiza wananchi kutokatishwa tamaa na baadhi ya viongozi wanaowataka wasichangie shughuli za maendeleo

Amesema kumekuwepo na baadhi ya viongozi ambao hawaitakii mema nchi hii kwa kuwadanganya wananchi wasishiriki kuchangia shughuli za maendeleo kwa madai kuwa serikali ndiyo pekee yenye jukumu hilo hivyoa wasubiri hadi itakavyowaletea

Jengo hilo lililogharimu kiasi cha shilingi milioni 36,112,400/= linatarajiwa kutoa huduma bora kwa wananchi wa kata hiyo ukizingatia kata hiyo ni miongoni mwa kata mpya wilayani hapo

Awali akisoma taarifa ya ujenzi huo afisa mtendaji wa kata ya Tandala Ambele Sanga amesema ujenzi huo umeshirikisha wananchia ambapo wananchi wamechangia sh. 16,112,400/= na kiasi kilichosalia cha sh. 20,000,000/= kimetolewa na halmashauri ya wilaya ya Makete

Ujenzi huo ulioanza Desemba 12,2013 unaendelea vizuri

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...