Naibu waziri wa Fedha Mhe. Saada Mkuya Salum mwishoni mwa juma alifanya ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa barabara za Kaskazini Pemba zenye urefu wa Kilomita 35. Ujenzi wa barabara hizi unafadhiliwa na Serikali ya Marekani kupitia programu ya Milennium Challenge Account – Tanzania (MCA-T) kwa thamani ya shilingi bilioni 38.2.
Mkataba wa ujenzi wa barabara hizi ulisainiwa tarehe 18 August, 2011 na unatekelezwa na kampuni ya ujenzi ya H. Young & Co(E.A) Ltd.
Ujenzi huu unajumuisha barabara za Kipangani - Kangagani (km 2.7), Chwale- Likoni (km 1.9), Mzambarauni Takao- Finya (km 7.9), Mzambarauni Karim - Mapofu (km 8.7), Bahanasa - Daya (km 6.7) na Makongeni – Daya - Mtambwe (km 7.1). 
Utekelezaji wa miradi hii uko katika hatua za kukamilika ambapo awali mradi huu ulitakiwa ukamilike tarehe 21 Machi, 2013 lakini kutokana na “contractor” ameomba aongezewe muda wa kukamilisha hadi tarehe 26 Desemba, 2013. 
Aidha, katika ziara hii Mhe. Naibu Waziri aliambatana na Mhe. Rajabu M. Mohamed (Mbunge wa Ole), Mhe. Haroub M. Shamin (Mbunge wa Chonga), Mhe. Rukia K. Ahmed (Mbunge Viti Maalum), Watendaji kutoka MCA-T, Wizara ya Fedha na Miundombinu – SMZ. 
 Wizara ya Fedha ya Serikali ya Muungano wa Tanzania ndiyo yenye jukumu la kuratibu utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa kupitia programu ya Milennium Challenge Account – Tanzania (MCA-T).
 Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Saada M. Salum akimsikiliza mkandarasi wa ujenzi wa barabara za Kaskazini Pemba na mwakilishi wa Kampuni ya LASA moja ya kampuni zinazotekeleza  mradi huu ndugu R.D Sharma kuhusu ujenzi unavyoendelea.
 Ndugu R.D Sharma wa wa Kampuni ya LASA, akitoa ufafanuzi wa baadhi ya masuala mbele ya Mhe. Naibu Waziri
Injinia Salum Sasillo (aliyesimama) kutoka MCA-T akitoa ufafanuzi. Injinia Sasillo ndiye mratibu wa utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara chini ya programu ya MCA-T

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...